Yobu 27 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Yobu akaendelea kutoa masemi yake, akasema:

2Kama vile Mungu anavyoishi,

aliyeniondolea haki yangu,

Mungu Mwenye Uwezo aliyeifanya nafsi yangu ikuwe na uchungu,

3ninaapa kwamba kadiri ninavyoweza kupumua,

roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu,

4midomo yangu haitasema uongo hata kidogo,

wala ulimi wangu kusema udanganyifu.

5Siwezi kabisa kusema kwamba ninyi munasema ukweli.

Mpaka kufa kwangu ninasema sina kosa.

6Ninashikilia haki yangu, wala sitaiacha;

katika zamiri yangu sina cha kunihukumu katika maisha yangu.

7Adui yangu apate azabu ya mwovu,

anayesimama kunishambulia aazibiwe kama mubaya.

8Asiyemwogopa Mungu ana tumaini gani

wakati Mungu anapokata pumzi yake,

anapomwondolea uzima wake?

9Wakati atakapopatwa na taabu,

Mungu atasikia kilio chake?

10Mwovu hawezi kufurahi mbele ya Mungu Mwenye Uwezo;

hataweza kudumu akimwomba Mungu.

11Nitawafundisha jinsi kitendo cha Mungu kinavyokuwa,

sitawaficha mipango ya Mungu Mwenye Uwezo.

12Lakini ninyi munajua jambo lile vizuri sana!

Mbona, basi munasema maneno yasiyokuwa na maana?

13Hiki ndicho Mungu alichomwekea mutu mwovu;

mutesaji alichopangiwa kupata ni hiki:

14Watoto wake hata wakuwe wengi watauawa kwa upanga;

wazao wake hawatakuwa na chakula cha kutosha.

15Wale watakaopona watakufa kwa ugonjwa mukali,

na wajane wao hawatawaomboleza.

16Hata akilundika feza kama vile mavumbi,

na nguo kama vile udongo wa mufinyanzi,

17yeye alundike tu, lakini mwenye haki ndiye atakayezivaa,

na feza yake watu wasiokuwa na kosa wataigawanyana.

18Nyumba mwovu anayojenga ni kama vile utando wa buibui,

ni kama vile kibanda cha mulinzi katika shamba.

19Anakwenda kulala akiwa tajiri, lakini ni mara ya mwisho;

atafungua macho yake, na utajiri wake umetoweka!

20Vitisho vinamufikia kama vile mafuriko;

usiku anapatwa na zoruba.

21Upepo mukali wa mashariki unamupeperusha naye anatoweka;

unamufagilia mbali kutoka makao yake.

22Upepo ule unamufunika bila huruma;

anajaribu kukimbia lakini mbio za bure.

23Upepo unamupigia vigelegele anapokimbia,

na kumuzomea toka pahali pake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help