1Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mumoja chetezo chake, wakaweka moto na ubani, wakamutolea Yawe moto usioruhusiwa, ambao haukulingana na agizo la Yawe.
2Basi, moto ukatokea mbele ya Yawe, ukawateketeza hao vijana, wakakufa mbele yake.
3Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.
4Basi, Musa akawaita Misaeli na Elisafani, wana wa Uzieli, baba mudogo wa Haruni, akawaambia wakuje kuondoa maiti za wandugu zao kutoka Pahali Patakatifu na kuzipeleka inje ya kambi.
5Wakatwaa maiti za wandugu zao na kuzipeleka inje ya kambi wakiwa wamevaa nguo zao, kama vile Musa alivyoamuru.
6Kisha Musa akamwambia Haruni na wana wake, Eleazari na Itamari: Musivuruge nywele zenu wala musipasue nguo zenu kwa kuomboleza, kama sivyo mutakufa na kuwaletea Waisraeli wote pamoja kasirani ya Yawe. Lakini wandugu zenu, ni kusema jamii yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo Yawe alioleta.
7Musitoke inje ya mulango wa hema la mukutano, kama sivyo mutakufa. Maana mafuta ya kupakaa ya Yawe yangali juu yenu. Haruni na wana wake wakafanya kama vile Musa alivyosema.
8Yawe akaongea na Haruni, akasema:
9Munapoingia ndani ya hema la mukutano, wewe na wana wako musikunywe divai wala kileo chochote, kama sivyo mutakufa. Hili litakuwa sharti ambalo vizazi vyenu vyote wanapaswa kulifuata siku zote.
10Munapaswa kuweka tofauti kati ya mambo matakatifu na mambo yasiyokuwa matakatifu, kati ya mambo machafu na yasiyokuwa machafu.
11Mutawafundisha Waisraeli masharti yote ambayo nimewaambia kwa njia ya Musa.
12Musa akamwambia Haruni na wana wake waliobakia, Eleazari na Itamari: Mutwae ile sehemu ya sadaka ya vyakula iliyobakia kutoka sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Muikule karibu na mazabahu bila kutiwa chachu kwa sababu ni takatifu kabisa. Ang. Law 6.14-18
13Mutaikula katika Pahali Patakatifu kwa sababu hiyo ni haki yako na wazao wako kutoka katika sadaka Yawe anazotolewa kwa moto. Hivi ndivyo nilivyoamuriwa.
14Lakini kilali ambacho wanafanya nacho kitambulisho cha kumutolea Yawe na muguu unaotolewa sadaka kama vile kitambulisho, munaweza kuvikulia pahali popote pasipo kuwa pachafu. Utakula wewe na watoto wako wanaume na wanawake. Vitu hivyo umepewa kama haki yako na ya wazao wako kutoka sadaka za amani za watu wa Israeli. Ang. Law 7.30-34
15Ule muguu uliotolewa na kilali cha sadaka ya kufanyia kitambulisho cha kumutolea Yawe watavileta pamoja na sadaka za mafuta zinazotolewa kwa moto, kwa kufanya kitambulisho cha kuvitolea mbele ya Yawe, vikuwe sadaka ya kutolewa kwa kitambulisho. Hivyo vitakuwa vyako pamoja na wana wako; ni haki yenu milele kama vile Yawe alivyoamuru.
16Basi, Musa akachunguza kwa uangalifu juu ya mbuzi mumoja aliyetolewa sadaka kwa ajili ya zambi, akatambua kwamba alikwisha kuteketezwa kwa moto. Hivyo akawakasirikia sana Eleazari na Itamari, wana wa Haruni waliobakia, akawauliza:
17Kwa nini hamukumukula katika Pahali Patakatifu kwa vile huyo ni kitu kitakatifu kabisa na mulikuwa mumepewa huyo kwa kuondoa kosa ya Waisraeli wote pamoja na kuwafanyia ibada ya upatanisho mbele ya Yawe? Ang. Law 6.24-26
18Tena, kwa vile damu yake haikuletwa ndani ya Pahali Patakatifu, mulipaswa kumukulia ndani ya Pahali Patakatifu kama vile nilivyoamuru.
19Haruni akamwambia Musa: Angalia, leo wametolea sadaka yao ya kuondoa zambi na sadaka ya kuteketezwa mbele ya Yawe; hata hivyo mambo haya yamenipata! Tena kama ningekula ile sadaka kwa ajili ya zambi hivi leo, ingekubalika mbele ya Yawe?
20Musa aliposikia hayo, akafurahi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.