2 Samweli 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Daudi na Mefiboseti

1Siku moja, Daudi aliuliza: “Hakuna hata mutu mumoja aliyebakia katika jamaa ya Saulo? Kama yuko, ningependa kumutendea mema kwa ajili ya Yonatani.”

2Kulikuwa mutumishi wa jamaa ya Saulo aliyeitwa Siba. Siba aliitwa kwenda kwa Daudi.

Mufalme Daudi alimwuliza: “Wewe ndiwe Siba?”

Naye akamujibu: “Ndiyo, mimi mutumishi wako ndiye.”

3Mufalme akamwuliza: “Hakuna hata mutu mumoja aliyebaki katika jamaa ya Saulo? Kama yuko, ningependa kumutendea wema wa Mungu.”

Siba akamujibu: “Kuko mwana wa Yonatani. Yeye ni kilema.”

4Mufalme akamwuliza: “Yuko wapi?”

Siba akamujibu: “Yuko kwenye nyumba ya Makiri mwana wa Amieli kule Lodebari.”

5Basi, mufalme Daudi akatuma watu, naye akaletwa kutoka nyumba ya Makiri mwana wa Amieli kule Lodebari.

6Basi, Mefiboseti mwana wa Yonatani na mujukuu wa Saulo akaenda kwa mufalme Daudi, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme Daudi. Daudi akamwita: “Mefiboseti!”

Naye akamujibu: “Ndiyo! Mimi mutumishi wako niko hapa.”

7Daudi akamwambia: “Usiogope. Mimi nitakutendea mema kwa ajili ya baba yako Yonatani. Nitakurudishia yale mashamba yote yaliyokuwa ya babu yako Saulo. Nawe, utakula kwenye meza yangu siku zote.”

8Mefiboseti akainama, na kusema: “Mimi ni sawa na imbwa mufu. Kwa nini unishugulikie hivyo?”

9Kisha, mufalme Daudi akamwita Siba mutumishi wa Saulo, akamwambia: “Ile mali yote iliyokuwa ya Saulo na jamaa yake nimemupa mujukuu wa bwana wako.

10Wewe, watoto wako na watumishi wako mutakuwa munamulimia Mefiboseti na mutamuletea mavuno kusudi mujukuu wa bwana wako akuwe na chakula siku zote. Lakini yeye atakula kwa meza yangu.” Wakati ule, Siba alikuwa na wana kumi na watano na watumishi makumi mbili.

11Kisha, Siba akamwambia mufalme: “Mimi mutumishi wako, nitafanya yote kulingana na amri yako.”

Basi, Mefiboseti akakuwa anapata chakula chake kwenye meza ya Daudi, kama vile mumoja wa watoto wa mufalme.

12Mefiboseti alikuwa na mwana mudogo aliyeitwa Mika. Watu wote wa jamaa ya Siba wakakuwa watumishi wa Mefiboseti.

13Kwa hiyo, Mefiboseti aliyekuwa kilema wa miguu yake yote akakuwa anaishi katika Yerusalema, na kupata chakula chake kwenye meza ya mufalme siku zote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help