1“Kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, na kushika kwa uangalifu amri ambazo ninawaamuru leo, yeye atawaweka juu ya mataifa yote katika dunia.
2Kama mukitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, mutapewa baraka hizi:
3“Miji yenu itabarikiwa na mashamba yenu.
4“Mutabarikiwa mupate wazao wengi, mavuno mengi, ngombe na kondoo wengi.
5“Vikapu vyenu vya ngano vitabarikiwa na vyombo vyenu vya kupondea mukate.
6Mutabarikiwa munaporudi kwa nyumba na munapotoka inje.
7Waadui zenu wakiwashambulia, Yawe atawapa ushindi juu yao. Wakikuja kuwashambulia kwa njia moja watawakimbia kwa njia saba.
8Baraka za Yawe zitakuwa katika gala zenu za ngano na katika shuguli zenu zote. Atawabariki katika inchi ambayo anawapa.
9“Yawe atawafanya kuwa watu wake watakatifu kama vile alivyowaahidi, kama mukitii amri zake yeye Yawe, Mungu wenu, na kufuata njia zake.
10Mataifa yote katika dunia yakiona kwamba ninyi munaitwa kwa jina la Yawe yatawaogopa.
11Yawe atawafanikisha kwa wingi: watoto, mifugo na mavuno katika shamba katika inchi aliyowaapia wazee wenu kwamba atawapa.
12Yawe atawafungulia hazina yake nzuri kutoka mbinguni na kunyesha mvua katika inchi kwa wakati wake, na kubariki kazi zenu. Mutakopesha mataifa mengi, lakini ninyi hamutakopa.
13Yawe, Mungu wenu, atawafanya kuwa wa kwanza kwa nguvu na sio wa mwisho. Mutaendelea mbele na sio kurudi nyuma kama mukishika amri zake ambazo ninawapa leo na kuwa waangalifu kwa kuzitimiza,
14bila kugeuka kuume au kushoto kwa kufuata miungu mingine na kuitumikia.
Kukosa utii(Law 26.14-46)15“Lakini kama hamutaitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, kama hamutakuwa waangalifu kushika amri zake zote na masharti ninayowaamuru leo, basi mutapatwa na laana hizi zote:
16Mutapata laana katika miji yenu na mashamba yenu.
17Vikapu vyenu vya ngano vitalaaniwa na vyombo vyenu vya kupondea mukate.
18Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya inchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.
19Mutalaaniwa munapoingia na munapotoka.
20“Yawe atawatumia laana, mashaka na kukata tamaa katika shuguli zenu zote mpaka muangamie upesi kwa sababu ya uovu wa matendo yenu na kwa sababu ya kumwacha Yawe.
21Atawaletea ugonjwa mukali mpaka ninyi wote muangamie kabisa katika inchi ambayo munaenda kurizi.
22Yawe atawashambulia kwa kifua kikuu, homa, majipu, joto kali, ukavu, zoruba na ukungu; mambo hayo yatawaandama mpaka muangamie.
23Mbingu zitakauka kama shaba nyeusi bila mvua, na inchi itakuwa kama chuma.
24Yawe ataifanya vumbi na muchanga kuwa mvua yenu, vumbi itawanyeshea mpaka muangamie.
25“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.
26Maiti zenu zitakuwa chakula cha ndege wala hakutakuwa mutu atakayewafukuza.
27Yawe atawapiga kwa majipu yaliyowapata Wamisri, atawapa vidonda, upele na kuwashwa ambavyo hamuwezi kuponywa.
28Yawe atawapiga kwa pigo la kuwa na wazimu, mutakuwa vipofu na kuvurugika akili.
29Mutakwenda kwa kupapasapapasa muchana kama vipofu wala hamutafanikiwa katika shuguli zenu. Mutakuwa munateswa kila mara na hakutakuwa mutu wa kuwasaidia.
30“Mutachumbia wabinti lakini watu wengine watalala nao. Mukijenga nyumba watu wengine watakaa ndani yake. Mukipanda mizabibu watu wengine watavuna.
31Ngombe wenu watachinjwa mbele ya macho yenu lakini hamutaonja hata kipande cha nyama yao. Punda wenu watatwaliwa kwa nguvu mbele ya macho yenu wala hamutarudishiwa. Kondoo wenu watapewa waadui zenu, na hakuna mutu atakayeweza kuwasaidia.
32Watoto wenu wanaume na wanawake watatolewa kwa watu wengine nanyi mutakodoa macho muchana kutwa kuwatazamia warudi, lakini hamutakuwa na nguvu ya kufanya chochote.
33“Taifa musilolijua litatwaa mazao yote ya inchi yenu na matunda ya jasho lenu, nanyi mutapondwa na kuteswa siku zote,
34hata mutapata wazimu kwa mambo mutakayoona kwa macho yenu wenyewe.
35Yawe atashambulia magoti yenu na miguu yenu kwa majipu makali ambayo hamutaweza kuponywa; yatawaenea tangu juu ya kichwa mpaka kwenye vikanyagio vya miguu.
36“Yawe atawapeleka ninyi na mufalme wenu mutakayejichagulia, mpaka kwa taifa ambalo ninyi hamukulijua wala wazee wenu. Na huko mutatumikia miungu mingine ya miti na mawe.
37Nanyi mutakuwa kinyaa, mazarau na mushangao kati ya watu wote wa inchi ambako Yawe atawapeleka.
38Mutapanda mbegu nyingi lakini mutavuna kidogo tu kwa sababu nzige watakula mazao yenu.
39Mutapanda mizabibu na kuitunza, lakini hamutavuna mizabibu hiyo wala kunywa divai yake, maana wadudu wataikula.
40Mutakuwa na mizeituni pahali pote katika inchi yenu, lakini hamutakuwa na mafuta ya kujipakaa, kwa sababu zeituni hizo zitaangukaanguka.
41Mutazaa watoto wanaume na wanawake, lakini hawatakuwa wenu, watapelekwa katika uhamisho.
42Matunda yenu yote na mazao yenu katika mashamba vitashambuliwa na nzige.
43“Wageni wanaoishi katika inchi yenu watazidi kupata nguvu wakati ninyi mutazidi kufifia zaidi na zaidi.
44Wao watawakopesha ninyi, lakini ninyi hamutakuwa na uwezo wa kuwakopesha. Wao watakuwa wa kwanza kwa nguvu nanyi mutakuwa wa mwisho.
45“Hayo yote yatawapata ninyi na kuwaandama mpaka muangamie kwa sababu hamukutii sauti ya Yawe, Mungu wenu, juu ya kushika amri zake na masharti aliyowapa.
46Lakini hizo zitakuwa ushuhuda wa hukumu ya Yawe kwenu na wazao wenu milele.
47“Yawe, Mungu wenu aliwabariki katika kila njia, lakini ninyi hamukumutumikia kwa moyo wa furaha na shangwe.
48Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.
49“Yawe ataleta kutoka mbali taifa moja liwashambulie mbio kama tai, taifa ambalo hamujui luga yake.
50Watu wa taifa hilo watakuwa na nyuso kali. Hawatajali wazee wala kuwahurumia vijana.
51Watakula ngombe wenu na mazao yenu, mpaka muangamie. Hawatawaachia ngano, divai, mafuta, ngombe au kondoo mpaka wawaangamize.
52Watu hao watawazunguka katika miji yenu yote, mpaka kuta zenu za makimbilio ambazo mulitegemea zimeporomoshwa chini kila pahali katika inchi yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa.
53Wakati wa kuzungukwa na kutaabishwa na waadui zenu, mutakula watoto wenu ambao Yawe, Mungu wenu, amewapa.
54Hata mutu mupole kabisa na aliyelelewa vizuri sana hatafurahi kuona ndugu yake, muke wake aliyemupenda na mutoto wake atakayebakia,
55wala hatamugawanyia hata mumoja wao nyama ya watoto wake atakaowakula. Hamutabakiliwa na chochote wakati huo wa kuzungukwa na kutaabishwa na waadui katika miji yenu yote.
56Hata mwanamuke yule ambaye ni mupole sana na aliyelelewa vizuri na mwenye kupendeza ambaye hajasubutu kukanyaga udongo kwa kikanyagio chake, hatafurahi kuona mume wake aliyemupenda na watoto wake. Wakati huo wa kuzungukwa kutakuwa njaa hata
57atakula mutoto wake muchanga kwa siri nyuma ya kumuzaa pamoja na nyama ya kizazi kwa sababu ya ukosefu wa chakula.
58“Kama musipokuwa waangalifu kwa kushika maneno yote ya sheria hii iliyoandikwa katika kitabu hiki na musipoheshimu na kutukuza jina tukufu la kuogopesha la Yawe, Mungu wenu
59basi, Yawe atawaletea ninyi na wazao wenu mateso yasiyokuwa ya kawaida, mateso makali yasiyoponyeshwa na ya kudumu, na magonjwa makali ya kudumu.
60Atawaletea tena yale magonjwa muliyoyaogopa katika inchi ya Misri, nayo yatawaandama siku zote.
61Atawaletea magonjwa ya kila aina na mateso mengine ambayo hayakutajwa katika kitabu hiki cha sheria mpaka muangamie.
62Ijapokuwa ninyi ni wengi kama nyota za mbinguni, lakini mutakuwa wachache tu kwa sababu hamukutii sauti ya Yawe, Mungu wenu.
63Kama vile Yawe alivyopendezwa kuwafanikisha na kuwafanya kuwa wengi, ni vile vile Yawe atapendezwa kuwaletea hasara na kuwaangamiza. Nanyi mutaondolewa katika inchi hiyo ambayo munakwenda kuirizi.
64Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.
65Hamutakuwa na raha yoyote pahali penu wenyewe pa kutulia wala kati ya mataifa hayo. Lakini Yawe atawapa huko wasiwasi wa moyo, kufifia kwa macho na mahangaiko ya ndani ya roho.
66“Maisha yenu yatakuwa katika mashaka, muchana na usiku mutakuwa na hofu na hamutakuwa na usalama wa maisha.
67Mioyo yenu itajaa woga wa kila kitu mutakachoona. Asubui mutasema ‘Heri ingekuwa magaribi’; magaribi itakapofika mutasema ‘Heri ingekuwa asubui’.
68Yawe atawarudisha Misri kwa mashua, safari ambayo aliahidi kwamba hamungeifanya tena. Huko mutajaribu kujiuzisha kwa waadui zenu kuwa watumwa, lakini hakuna mutu atakayewanunua.”
69Haya ni maneno ya agano ambalo Yawe aliwaamuru Musa kufanya na Waisraeli katika inchi ya Moabu, zaidi ya agano Yawe alilofanya nao kwenye mulima Horebu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.