Waamuzi 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wamidiani wanashindwa kabisa

1Watu wa kabila la Efuraimu wakamwuliza Gideoni: “Kwa nini umetutendea hivyo? Kwa nini haukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakamugombeza kwa ukali.

2Lakini Gideoni akawajibu: “Mambo niliyofanya mimi si kitu kabisa yakilinganishwa na yale muliyoyafanya ninyi. Walichookota watu wa Efuraimu wakati wa mavuno ni kizuri kuliko mavuno ya jamaa yangu ya Abiezeri.

3Mungu amewatia katika mikono yenu wale wakubwa wa Midiani, Kibombobombo na Imbwa-wa-Pori. Basi, mimi nimefanya nini nikilinganishwa nanyi?” Gideoni alipokwisha kusema hivyo, hasira yao juu yake ikatulia.

4Gideoni na wenzake mia tatu wakafika Yordani, wakavuka. Ingawa walikuwa wamechoka sana, waliendelea kuwafuatilia waadui zao.

5Basi, akawaambia watu wa Sukoti: “Tafazali, muwape wenzangu hawa mikate maana wamechoka sana; nami ninaendelea kuwafuatilia Sadaka na Kivuli, wafalme wa Midiani?”

6Lakini viongozi wa Sukoti wakamwuliza: “Kwa nini tuwape mikate nanyi hamujamushinda Sadaka na Kivuli?”

7Gideoni akawaambia: “Sawa, lakini Yawe atakapowatia Sadaka na Kivuli katika mikono yangu, nitaichanachana miili yenu kwa miiba na michongoma za jangwa.”

8Kutoka kule akawaendea watu wa Penueli, akawaomba namna ileile. Nao watu wa Penueli wakamujibu kama vile watu wa Sukoti walivyomujibu.

9Gideoni akawaambia: “Nitakaporudi kwa amani nitaubomoa munara huu.”

10Sadaka na Kivuli walikuwa kule Karkori pamoja na jeshi lao la watu elfu kumi na tano ambao ndio tu waliobaki kutoka jeshi la upande wa mashariki, maana wenzao elfu mia moja na makumi mbili waliuawa.

11Gideoni akafuata njia ya upande wa magaribi inayokuwa upande wa mashariki wa Noba na Yogibeha, akalishambulia jeshi hilo ambalo halikukuwa tayari.

12Sadaka na Kivuli, wafalme wa Midiani, walitoroka wakakimbia, lakini Gideoni akawafuatilia, akawakamata na kulitia jeshi lote hofu kubwa.

13Kisha, Gideoni mwana wa Yoasi, akarudi kutoka katika vita akipitia kwenye muteremuko wa Heresi.

14Akamukamata kijana mumoja wa Sukoti na kumwulizauliza. Kijana huyo akamwandikia majina ya viongozi na wazee wakubwa wa Sukoti, jumla yao watu makumi saba na saba.

15Gideoni akarudi kwa watu wa Sukoti, akawaambia: “Si mutakumbuka mulivyonitukana muliposema: ‘Kwa nini tuwape mikate watu wako waliochoka sana nanyi hamujamushinda Sadaka na Kivuli?’ Haya basi, Sadaka na Kivuli ndio hawa.”

16Basi, akawatwaa wazee wa Sukoti na kuwapa fundisho wanaume wote kwa kuichana miili yao kwa miiba na michongoma.

17Vilevile akaubomoa munara wa Penueli na kuwaua wakaaji wa muji ule.

18Kisha, akawauliza Sadaka na Kivuli: “Watu wale muliowaua kule Tabori walikuwa namna gani?”

Wakamujibu: “Walifanana na wewe, maana walionekana kama wana wa mufalme.”

19Naye akawaambia: “Hao walikuwa wandugu zangu, wana wa mama yangu muzazi. Kama vile Yawe anavyoishi, kama musingewaua, hata mimi nisingewaua ninyi.”

20Kisha akamwambia Yeteri, muzaliwa wake wa kwanza: “Simama, uwaue.” Lakini Yeteri akaogopa kutwaa upanga wake maana alikuwa angali kijana.

21Hapo Sadaka na Kivuli wakasema: “Utuue wewe mwenyewe, maana hii ni kazi ya mutu muzima.”

Gideoni akawaua yeye mwenyewe na kutwaa mapambo yao yaliyokuwa kwenye shingo la ngamia wao.

22Kisha, Waisraeli wakamwambia Gideoni: “Wewe ukuwe mutawala wetu, na nyuma yako wazao wako watutawale, kwa sababu wewe umetukomboa kutoka kwa Wamidiani.”

23Gideoni akawajibu: “Mimi sitakuwa mutawala wenu wala mwana wangu hatakuwa mutawala wenu. Yawe ndiye atakayekuwa mutawala wenu.”

24Kisha akawaambia: “Ningependa kuwaomba kitu kimoja; ninaomba kila mumoja wenu anipe pete kati ya vitu mulivyoteka.” Wale Wamidiani kwa vile walikuwa Waisimaeli, walivaa pete za zahabu.

25Watu wakamujibu: “Tutakupa pasipo kunungunika.” Wakatandaza nguo na kila mumoja akatupa pale pete walizokuwa wameteka.

26Uzito wa pete zote alizoomba wamupe ulikuwa kilo makumi mbili. Zaidi ya hivyo, alipokea vilevile vyuma vya masikio, nguo za rangi nyekundu-nyeusi zilizovaliwa na wafalme wa Midiani na mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia wao.

27Gideoni akazitumia kwa kutengenezea kizibao ambacho alikiweka kwenye muji wake wa Ofura. Waisraeli wote wakaenda kule kukiabudu. Kizibao hicho kikakuwa mutego kwa Gideoni na jamaa yake.

28Basi, Wamidiani walishindwa kabisa nao hawakuweza kujiinua juu hata kidogo.

Inchi ya Israeli ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi ine.

Kifo cha Gideoni

29Gideoni, ni kusema Yerubali mwana wa Yoasi, akarudi kwake na kukaa kule.

30Gideoni alikuwa na watoto wanaume makumi saba, maana alioa wanawake wengi.

31Alikuwa na habara kule Sekemu ambaye alimuzalia mutoto mwanaume, jina lake Abimeleki.

32Gideoni mwana wa Yoasi, akakufa akiwa na umri mukubwa, akazikwa katika kaburi la baba yake Yoasi kwenye muji wa Ofura wa Waabiezeri.

33Nyuma ya kifo cha Gideoni, Waisraeli wakairudilia miungu ya Bali na kuiabudu. Wakamufanya Bali-Beriti kuwa mungu wao.

34Waisraeli wakamusahau Yawe, Mungu wao, aliyewakomboa kutoka kwa waadui zao wengi waliowazunguka kila upande.

35Tena, hawakuitendea mema jamaa ya Yerubali, ni kusema Gideoni kwa mema yote aliyoyatenda katika Israeli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help