Ezekieli 35 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Unabii juu ya Edomu

1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

2Wewe mwanadamu! Ugeukie upande wa mulima Seiri, utoe unabii juu ya wakaaji wake.

3Uwaambie kwamba:

Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi ninapingana nawe, ee mulima Seiri. Ninanyoosha mukono wangu juu yako na kukufanya ukuwe jangwa na ukiwa.

4Ninaifanya miji yako kuwa mabomoko nawe utakuwa jangwa. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.

5Ulikuwa adui wa siku zote wa Waisraeli, ukasababisha watu wake wauawe kwa upanga, wakati wa musiba wao, wakati wa azabu yao ya mwisho.

6Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– kifo kinakungoja na hautaweza kukiepuka. Uko na makosa ya mauaji, basi mauaji nayo yatakuandama.

7Nitaufanya mulima Seiri kuwa ukiwa na jangwa na yeyote atakayepitia huko nitamwangamiza.

8Nitajaza milima yako watu waliouawa; na katika vilima vyako na mabonde yako na mitelemuko yako yote kutakuwa watu waliouawa kwa upanga.

9Nitakufanya kuwa jangwa milele, na miji yako haitakaliwa tena. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.

10Wewe ulisema kwamba mataifa hayo mawili, ni kusema inchi ya Yuda na ya Israeli, ni mali yako na kwamba utazirizi! Ulisema hivyo ingawa humo ni makao yangu mimi Yawe.

11Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nitakutendea kadiri ya hasira na wivu wako, kulingana na chuki yako kwao. Nitakapokuazibu utatambua mimi ni nani!

12Wewe utajua kwamba mimi mwenyewe Yawe nimeyasikia matusi yote uliyoyatoa juu ya milima ya Waisraeli, ukisema: Milima ya Israeli imefanywa kuwa jangwa! Imetolewa kusudi tupate kuinyanganya!

13Nimesikia jinsi unavyojivuna na kusema maneno mengi juu yangu.

14Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakapokufanya wewe Edomu kuwa jangwa, dunia yote itafurahi

15kama wewe ulivyofanya wakati inchi ya Waisraeli ilipoharibiwa. Utakuwa jangwa, ewe mulima Seiri, pamoja na inchi yote ya Edomu. Halafu watu watatambua kwamba mimi ni Yawe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help