Mika 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mutawala mupya kutoka Betelehemu

1Yawe anasema hivi:

Lakini wewe Betelehemu katika Efurata,

wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda,

lakini kwako kutanitokea mutawala

atakayetawala juu ya Israeli.

Asili yake ni ya zamani sana.

2Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui,

mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa.

Kisha wandugu zake waliobakia,

watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.

3Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe,

kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake.

Watu wake wataishi kwa usalama,

maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.

4Yeye ndiye atakayeleta amani.

Ukombozi na azabu

Waasuria wakishambulia inchi yetu,

na kuingia katika nyumba zetu nzuri,

tutatuma walinzi wetu wapigane nao,

tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.

5Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria,

na kuirizi inchi ya Nimurodi.

Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria,

watakapoingia katika inchi yetu

na kuanza kuishambulia.

6Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima

wataenea kati ya mataifa mengi,

watakuwa kama umande unaotoka kwa Yawe,

kama manyunyu yanayoanguka kwenye majani

ambayo hayasababishwi na mutu

wala kumutegemea mwanadamu.

7Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima,

wataenea kati ya mataifa na watu wengi

watakuwa na nguvu kubwa

kama simba kati ya nyama wa pori,

kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo,

ambaye kila pahali anapopita,

anarukia na kurarua nyama,

na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.

8Waisraeli watawashinda waadui zao

na kuwaangamiza kabisa.

9Wakati ule,

nitawaondoa farasi wenu,

na kuyaharibu magari yenu ya vita.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

10Nitaiharibu miji ya inchi yenu,

na kubomoa vikingio vyenu.

11Nitakomesha matendo yenu ya uchawi,

nanyi hamutakuwa tena na waaguzi.

12Nitaziharibu sanamu zenu,

na nguzo zenu za ibada;

nanyi mutakoma kuabudu vitu mulivyotengeneza wenyewe.

13Nitaziongoa sanamu za Ashera kutoka kwenu,

na kuiangamiza miji yenu.

14Kwa hasira na kasirani yangu,

nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help