1Yawe anasema hivi:
Lakini wewe Betelehemu katika Efurata,
wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda,
lakini kwako kutanitokea mutawala
atakayetawala juu ya Israeli.
Asili yake ni ya zamani sana.
2Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui,
mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa.
Kisha wandugu zake waliobakia,
watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.
3Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe,
kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake.
Watu wake wataishi kwa usalama,
maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.
4Yeye ndiye atakayeleta amani.
Ukombozi na azabuWaasuria wakishambulia inchi yetu,
na kuingia katika nyumba zetu nzuri,
tutatuma walinzi wetu wapigane nao,
tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.
5Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria,
na kuirizi inchi ya Nimurodi.
Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria,
watakapoingia katika inchi yetu
na kuanza kuishambulia.
6Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima
wataenea kati ya mataifa mengi,
watakuwa kama umande unaotoka kwa Yawe,
kama manyunyu yanayoanguka kwenye majani
ambayo hayasababishwi na mutu
wala kumutegemea mwanadamu.
7Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima,
wataenea kati ya mataifa na watu wengi
watakuwa na nguvu kubwa
kama simba kati ya nyama wa pori,
kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo,
ambaye kila pahali anapopita,
anarukia na kurarua nyama,
na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.
8Waisraeli watawashinda waadui zao
na kuwaangamiza kabisa.
9Wakati ule,
nitawaondoa farasi wenu,
na kuyaharibu magari yenu ya vita.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
10Nitaiharibu miji ya inchi yenu,
na kubomoa vikingio vyenu.
11Nitakomesha matendo yenu ya uchawi,
nanyi hamutakuwa tena na waaguzi.
12Nitaziharibu sanamu zenu,
na nguzo zenu za ibada;
nanyi mutakoma kuabudu vitu mulivyotengeneza wenyewe.
13Nitaziongoa sanamu za Ashera kutoka kwenu,
na kuiangamiza miji yenu.
14Kwa hasira na kasirani yangu,
nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.