1Sheria ya Kiyuda ni mufano wa mema yatakayotokea, lakini si kitambulisho kinachoonyesha mambo yale kamili. Kwa sababu hii Sheria haiwezi hata mara moja, kwa njia ya sadaka zinazotolewa mara nyingi kila mwaka, kuwafanya wakamilifu wale wanaomwendea Mungu.
2Wale wanaomwabudu Mungu kwa njia ile wangetakaswa kabisa kwa mara moja tu, nayo zamiri yao isingewahukumu tena hata kidogo juu ya zambi, basi sadaka zile hazingeacha kutolewa.
3Lakini kwa njia ya sadaka zile, watu wanakumbushwa zambi zao kila mwaka,
4kwa sababu damu ya ngombe na ya mbuzi haiwezi kuondoa zambi.
5Kwa sababu hii, wakati Kristo alipokuja katika dunia alisema:
“Wewe haukutaka sadaka wala matoleo.
Lakini umeniumbia mwili.
6Haukupendezwa na sadaka za kuteketezwa kwa moto
wala sadaka za kusamehewa zambi.
7Halafu nikasema: ‘Niko hapa, ee Mungu,
nimekuja kufanya mapenzi yako,
kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria.’ ”
8Kwanza Kristo alisema: “Haukutaka wala haukupendezwa na sadaka na matoleo, wala sadaka za kuteketezwa kwa moto wala sadaka za kusamehewa zambi.” (Alisema vile ingawa sadaka hizo zote zilitolewa kufuatana na maagizo ya Sheria.)
9Kisha akasema: “Mimi niko hapa, ee Mungu, nimekuja kufanya mapenzi yako.” Kwa hiyo Mungu ameondoa hizo sadaka zote za kwanza na kuzikomboa na Kristo mwenyewe kama sadaka.
10Na kwa sababu Yesu Kristo alifanya mapenzi ya Mungu, sisi tumetakaswa zambi kwa njia ya mwili wake alioutoa sadaka kwa mara moja tu.
11Kila kuhani anasimama mbele ya Mungu kila siku kwa kufanya ibada na kutoa sadaka za namna moja mara nyingi zisizoweza hata kidogo kuondoa zambi.
12Lakini Kristo yeye alitoa sadaka moja tu inayofaa kwa milele kwa ajili ya usamehe wa zambi. Na kisha akaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.
13Na kule anangoja sasa mpaka waadui zake wote watiwe chini ya miguu yake.
14Kwa maana kwa njia ya sadaka moja aliyotoa, amewafanya wale aliowatakasa kuwa wakamilifu hata milele.
15Naye Roho Mutakatifu anatushuhudia mambo hayo vilevile. Kwanza anasema maneno haya:
16“Hili ndilo agano nitakalofanya nao nyuma ya siku zile.
Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.
Nitawawezesha kuchunga sheria zangu
ndani ya mafikiri,
nikiziandika ndani ya mioyo yao.”
17Naye anaongeza kusema:
“Nami sitakumbuka tena zambi wala maovu yao.”
18Basi wakati zambi zinaposamehewa, hakuna tena hitaji la kutoa sadaka kwa ajili ya usamehe wa zambi.
Tumukaribie Mungu19Basi wandugu, tuko na uhodari wa kuingia katika Pahali Patakatifu kwa njia ya damu ya Yesu.
20Yeye ametufungulia njia mupya ya uzima, inayopitia katika pazia, maana yake mwili wake mwenyewe.
21Sisi tuko na Kuhani Mukubwa anayesimamia nyumba yote ya Mungu.
22Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.
23Tuendelee kuchunga lile tumaini tuliloshuhudia bila kuchoka, kwa maana Mungu aliyetupatia ahadi ni mwaminifu.
24Tena tushugulikiane kusudi tupate kuvutana sisi kwa sisi kuwa na upendo na kufanya mema.
25Tusiache kukusanyika pamoja, kama vile wamoja wanavyozoea kufanya. Lakini tuonyane, na zaidi sana kufuatana na vile munavyoona kwamba Siku ya Bwana inakaribia.
26Kwa maana tukifanya zambi kwa makusudi tukisha kutambua waziwazi ukweli, hakuna tena sadaka ingine inayoweza kutolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.
27Lakini inayobaki tu ni kungojea kwa woga hukumu na moto mukali wa Mungu utakaowateketeza waasi.
28Mutu yeyote aliyevunja Sheria ya Musa, aliuawa bila huruma kisha ushuhuda wa watu wawili au watatu.
29Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?
30Kwa maana tunamujua yule aliyesema: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.” Naye alisema tena: “Bwana atawahukumu watu wake.”
31Kuanguka katika mikono ya Mungu Mwenye Uzima ni jambo la kuogopa sana!
32Mukumbuke mambo yaliyowatokea katika siku zilizopita. Ninyi mulipokwisha kuangaziwa na Mungu, mulipita katika mateso mengi lakini mulivumilia.
33Kwa ngambo moja mulitukanwa na kuteswa waziwazi mbele ya watu. Na kwa ngambo ingine mulishirikiana na wale waliotendewa vibaya.
34Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.
35Basi musikate tumaini, kwa maana litawaletea zawadi kubwa.
36Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.
37Kwa maana, kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema:
“Kunabaki wakati kidogo sana,
yule anayepaswa kuja, afike
wala hatakawia.
38Mwenye haki mbele yangu
ataishi kwa njia ya imani.
Lakini kama akirudi nyuma, sitapendezwa naye.”
39Lakini sisi si watu wenye kurudi nyuma na kupotea, lakini sisi ni watu wenye imani na wenye kuokoka.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.