Zaburi 131 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kumutumainia Mungu kwa utulivu

1Wimbo wa safari za kidini: wa Daudi.

Ee Yawe, sina moyo wa majivuno;

wala macho yangu si ya kiburi.

Sijishugulishi na mambo makubwa,

yale yanayokuwa ya ajabu sana kwangu.

2Lakini nafsi yangu imetulia na kuwa na amani,

kama mutoto muchanga anavyotulia na mama yake;

ndivyo nafsi yangu inavyokuwa na utulivu.

3Ee Israeli, umutumainie Yawe,

tangu sasa na hata milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help