Waebrania 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Basi kwa kuwa tungali na ahadi ya kuingia kwenye mapumziko yale, basi tufanye angalisho kusudi katikati yenu kusikuwe hata mutu mumoja atakayekosa kuingia.

2Kwa maana sisi vilevile tumehubiriwa Habari Njema kama vile watu wale. Walisikia habari lakini haikuwafalia kitu, kwa maana wale walioisikia hawakuipokea kwa imani.

3Lakini sasa sisi tulioamini, tutaingia kwenye mapumziko ambayo Mungu alitaja aliposema:

“Halafu nikaapa kwa kasirani

kwamba hawataingia hata kidogo kwenye mapumziko niliyowatayarishia!”

Mungu alisema vile ingawa alikuwa amemaliza kazi zake tangu pale alipoumba dunia.

4Kwa maana imesemwa pahali fulani katika Maandiko Matakatifu juu ya siku ya saba: “Siku ya saba, Mungu akapumzika kwa maana alikuwa amemaliza kazi zake zote.”

5Na tena, katika Maandiko tuliyotaja hapa juu, Mungu anasema: “Hawataingia hata kidogo kwenye mapumziko niliyowatayarishia.”

6Wale waliokuwa wa kwanza kuhubiriwa Habari Njema hawakuingia kwenye mapumziko yale kwa sababu ya kutokuamini kwao. Ingawa vile ingali inawezekana kwa wengine kuingia.

7Kwa sababu hii Mungu anaweka tena siku ingine inayoitwa “Leo”. Naye alisema juu ya siku ile nyuma ya miaka mingi kwa njia ya Daudi, kufuatana na Maandiko haya yaliyokwisha kutajwa mbele:

“Leo kama munasikiliza sauti ya Mungu

musifanye mioyo yenu kuwa migumu.”

8Kwa maana kama Yoshua angekuwa amewafikisha watu kwenye mapumziko, Mungu hangesema tena nyuma ya pale juu ya siku ingine.

9Kwa hiyo kungali mapumziko ambayo Mungu anawatayarishia watu wake.

10Kwa maana yule anayeingia kwenye mapumziko anayotayarisha, anapumzika kwa kuwa amemaliza kazi zake zote kama vile Mungu alivyopumzika alipomaliza kazi zake.

11Basi tufanye bidii ya kuingia kwenye mapumziko yale, kusudi hata mutu mumoja asianguke sawa vile wale walioasi katika jangwa.

12Kwa maana Neno la Mungu ni lenye uzima, na lina nguvu; ni kali kupita upanga unaokata ngambo mbili. Linapenya hata linatenga moyo na roho na hata viungo na ubongo. Nalo linatambua nia na mawazo ya mutu.

13Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.

Yesu ni Kuhani Mukubwa zaidi

14Basi, kwa kuwa tuko na Kuhani Mukubwa zaidi aliyeingia mbinguni, ndiye Yesu Mwana wa Mungu, tushikamane sana na imani tunayotangaza.

15Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.

16Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help