1Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni anyooshe mukono wake na kuinua fimbo yake juu ya mito, juu ya mifereji na visima, nao vyura watatokea na kuenea kila pahali katika inchi ya Misri.”
2Basi, Haruni akainua fimbo yake juu ya maji yote. Vyura wakatokea na kufunika inchi nzima ya Misri.
3Lakini wachawi wa Misri kwa uchawi wao vilevile wakaleta vyura katika inchi ya Misri.
4Kisha mufalme wa Misri akamwita Musa na Haruni, akawaambia: “Musihi Yawe, kusudi aniondolee mimi na watu wangu vyura hawa, nami nitawaacha Waisraeli wajiendee na kutoa sadaka kwa Yawe.”
5Musa akamujibu mufalme wa Misri: “Basi! Unaweza kutaja wakati unaotaka nikuombee kwa Mungu, niwaombee wakubwa wako na watu wako. Nitamwomba awaangamize vyura hawa wanaokuwa katika nyumba zenu. Watabaki tu katika muto Nili!”
6Mufalme wa Misri akamwambia: “Kesho.”
Musa akasema: “Nitafanya kama vile unavyosema, kusudi ujue kwamba hakuna yeyote anayelingana na Yawe, Mungu wetu.
7Vyura wataondoka kwako, na kwenye nyumba zenu, kwa wakubwa wako na kwa watu wako. Watabaki tu katika muto Nili.”
8Basi, Musa na Haruni wakaondoka kwa nyumba ya mufalme wa Misri na Musa akamulilia Yawe amwondolee mufalme vyura wale aliomuletea.
9Yawe akafanya kama vile Musa alivyomwomba. Vyura wakakufa katika nyumba, viwanja na kwenye baraza za nyumba na katika mashamba.
10Watu wakawakusanya vyura wale malundomalundo. Inchi nzima ikanuka.
11Lakini mufalme wa Misri alipoona kwamba inchi imepata utulivu, akakuwa na moyo mugumu tena, wala hakusikiliza Musa na Haruni, kama vile Yawe alivyokuwa amesema.
Pigo la tatu: Chawa12Kisha, Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni ainue fimbo yake na kupiga mavumbi, nayo yatageuka kuwa chawa katika inchi yote ya Misri.”
13Musa na Haruni wakafanya hivyo. Haruni akainua fimbo yake na kupiga mavumbi, nayo yakageuka kuwa chawa nao wakakuwa juu ya watu na nyama. Mavumbi yote katika inchi yote ya Misri yakageuka kuwa chawa.
14Wachawi wa Misri, kwa uchawi wao, wakajaribu kuyageuza mavumbi yakuwe chawa, lakini hawakuweza. Chawa wale wakaenea juu ya watu na nyama.
15Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema. Pigo la ine: Mainzi
16Kisha Yawe akamwambia Musa: “Kesho amuka asubui mapema umwendee mufalme wa Misri wakati anapokwenda kwenye muto umwambie: ‘Yawe anasema hivi: Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.
17Kama ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitakuletea makundi ya mainzi, wewe, wakubwa wako na watu wako wote. Wataingia kwenye nyumba zenu na nyumba zote za Wamisri zitajaa makundi ya mainzi na inchi yote ya Misri vilevile.
18Lakini siku hiyo sehemu ya Goseni watu wangu wanakoishi nitaikinga. Kule mainzi wale hawatakuwa. Kwa hiyo utatambua kwamba mimi Yawe ninatenda mambo katika inchi yako.
19Nitakinga watu wangu na mambo yatakayowapata watu wako. Mambo hayo yatafanyika kesho.’ ”
20Yawe akafanya kama vile alivyosema. Makundi makubwa ya mainzi yakashambulia nyumba ya mufalme wa Misri, nyumba za wakubwa wake na inchi nzima ya Misri. Inchi nzima ya Misri ikaharibiwa na mainzi wale.
21Halafu mufalme wa Misri akawaita Musa na Haruni, akawaambia: “Munaweza kwenda kutoa sadaka kwa Mungu wenu, lakini ikuwe humuhumu katika inchi ya Misri.”
22Lakini Musa akamujibu: “Hapana! Haifai kufanya hivyo, maana sadaka tutakazomutolea Yawe, Mungu wetu, zitawachukiza Wamisri. Wamisri wakituona tunatoa sadaka ambazo ni chukizo kwao, si watatupiga mawe?
23Tusafiri mwendo wa siku tatu katika jangwa tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka kama vile atakavyotuamuru.”
24Basi, mufalme wa Misri akasema: “Nitawaacha mujiendee kutoa sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, katika jangwa. Lakini musiende mbali sana. Muniombee mimi.”
25Musa akamujibu: “Mara tu nitakapokuacha, kesho nitamwomba Yawe makundi haya ya mainzi yatoweke kwako wewe mufalme, wakubwa wako na watu wako. Lakini wewe usitudanganye tena kwa kukataa kuwaacha watu kwenda kutoa sadaka kwa Yawe.”
26Basi, Musa akaondoka kwa nyumba ya mufalme wa Misri, akamwomba Yawe.
27Yawe akafanya kama vile Musa alivyomwomba. Wale mainzi wakatoweka kutoka kwa mufalme wa Misri, wakubwa wake na watu wake, wala hakukubaki hata mumoja.
28Lakini hata mara hii mufalme wa Misri akafanya moyo wake kuwa magumu, wala hakuwaruhusu Waisraeli kuondoka.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.