1Rudia, rudia ewe binti Musulami.
Rudia, rudia tupate kukuangalia.
Masemi ya bintiKwa nini munataka kumwangalia Musulami
sawa vile munaangalia muchezo wa ngoma
kati ya makundi mawili?
Masemi ya mume2Miguu yako inapendeza sana katika viatu,
ewe binti wa kifalme.
Mizunguko ya kiuno chako ni kama ushanga,
kazi ya fundi hodari.
3Kitofu chako ni kama bakuli
lisilokosa divai iliyokolezwa.
Tumbo lako ni kama lundo la ngano
lililozungushiwa mayungiyungi pembeni.
4Maziba yako ni kama paa mapacha,
ni kama swala wawili.
5Shingo yako ni kama munara wa pembe za tembo.
Macho yako ni kama visima vya muji wa Hesiboni,
karibu na mulango wa Beti-Rabi.
Pua yako ni kama munara wa Lebanoni,
ambao unauelekea muji wa Damasiki.
6Kichwa chako ni kama mulima Karmeli.
Misuko ya nywele zako ni nyekundu-nyeusi.
Uzuri wako unaweza kumuvuta hata mufalme.
7Angalia jinsi sura yako ni nzuri na ya kuvutia,
ewe mupenzi, binti unayependeza!
8Umbo lako linapendeza kama muti wa ngazi,
maziba yako ni kama shada za ngazi.
9Nilisema nitapanda muti wa ngazi na kuchuma shada za ngazi.
Kwangu maziba yako ni kama shada za zabibu,
harufu nzuri ya pumzi yako ni kama matunda ya mutofaa;
10na kinywa chako ni kama divai tamu.
Masemi ya mukeBasi, divai itiririke mpaka kwa mupenzi wangu,
ipite juu ya midomo yake na meno yake!
11Mimi ni wa mupenzi wangu,
naye ananisikilia hamu sana.
12Kuja, ewe mupenzi wangu,
tuende katika mashamba,
tuende tulale kule katika vijiji.
13Tutaamuka mapema,
tuende kwenye mashamba ya mizabibu,
tuone kama imeanza kuchipuka,
na kama maua ya zabibu yamekwisha kuchanua,
vilevile kama mikomamanga imeanza kutoa maua.
Kule ndiko nitakapokupatia pendo langu.
14Harufu nzuri ya dudai imejaa katika hewa.
Karibu na milango yetu kuna kila aina ya matunda bora,
yote mapya na ya siku za nyuma,
ambayo nimekuwekea wewe mupenzi wangu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.