Amosi 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maono ya ine: Kikapu cha matunda

1Bwana wetu Yawe alinionyesha maono mengine: Niliona kikapu kilichojaa matunda yenye kuivya.

2Naye Yawe akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kikapu cha matunda yenye kuivya. Kisha Yawe akaniambia:

Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli.

Sitavumilia tena maovu yao.

3Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Kutakuwa maiti nyingi,

nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya. Mungu ataiazibu Israeli

4Musikilize, enyi munaowagandamiza wakosefu

na kuwaletea maangamizi wamasikini wa inchi.

5Munajisemesha ndani ya mioyo yenu:

Sikukuu ya mwandamo wa mwezi itakwisha wakati gani

kusudi tuanze tena kuuzisha vyakula vyetu?

Siku ya Sabato itakwisha wakati gani

kusudi tupate kuuzisha ngano yetu?

Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei,

tutadanganya watu kwa mizani zisizokuwa sawa.

6Tutawanunua wamasikini kwa feza

na wakosefu kwa bei ya muguu mumoja wa mapapa.

Nasi tutauzisha machenga ya ngano.

7Yawe, utukufu wa Yakobo, ameapa:

Hakika, sitayasahau matendo yao maovu.

8Kwa hiyo, dunia itatetemeka

na kila mutu katika inchi atafanya kilio.

Inchi yote itayumbayumba;

itapanda na kushuka,

kama vile maji ya muto Nili yanavyojaa na kupunguka!

9Siku hiyo,

nitalifanya jua litue pa saa sita za muchana,

na kuijaza inchi giza wakati wa muchana.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

10Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio,

na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo.

Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni

na kunyoa vichwa vyenu upaa,

kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee.

Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.

11Siku zinakuja

ambapo nitaleta njaa katika inchi.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Lakini si njaa ya kukosa chakula wala kiu ya kukosa maji,

lakini njaa ya kusikia maneno ya Yawe.

12Watu watatangatanga kutoka bahari hata bahari,

kutoka upande wa kaskazini mpaka wa mashariki.

Watakimbia huko na huko wakitafuta neno la Yawe,

lakini hawatalipata.

13Siku hiyo, wabinti wazuri na vijana wanaume

watazimia kwa kiu.

14Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria

na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani”

au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”,

wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help