Nehemia 7 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Nyuma ya ukuta kumalizika, milango yote kuwa tayari, na kuchaguliwa kwa walinzi wa milango, waimbaji na Walawi,

2nikamuchagua ndugu yangu Hanani kuwa mwangalizi wa Yerusalema akishirikiana na Hanania aliyekuwa jemadari wa waaskari walinzi wa munara katika Yerusalema; kwa sababu alikuwa mutu wa kutegemewa na anayemwogopa sana Mungu, hapakukuwa mwingine aliyelingana naye,

3nikawaagiza: “Milango isifunguliwe usiku kucha mpaka jua linapokuwa limepanda. Mbele ya kuondoka kwa walinzi ni lazima kufunga milango yote kwa vifungio vyake. Muchague walinzi kati ya wakaaji wa muji wa Yerusalema, kila mumoja akuwe kwa nafasi yake kuelekeana na nyumba yake.”

Hesabu ya watu waliorudi toka katika uhamisho(Ezra 2.1-70)

4Muji wa Yerusalema ulikuwa mupana na mukubwa, lakini wakaaji wake walikuwa wachache na nyumba zilikuwa hazijajengwa.

5Mungu akanipa moyo kuwakusanya viongozi na watu kwa kujua ukoo zao. Nikapata kitabu cha ukoo za watu waliorudi toka katika uhamisho mara ya kwanza, na hawa ndio waliokuwa wameandikwa ndani yake.

6Wale waliokuwa katika uhamisho kule Babeli, walirudi Yerusalema na katika inchi ya Yuda, kila mumoja akarudi katika muji wake. Jamaa zao walikuwa wamekaa Babeli tangu mufalme Nebukadneza alipowahamishia kule wakiwa watumwa.

7Waliporudi waliongozwa na Zerubabeli, Yesua, Nehemia, Azaria, Ramia, Nahamani, Mordekayi, Bilsani, Misipereti, Bigwayi, Nehumu na Bana. Hii ndiyo jumla ya watu wa ukoo za Waisraeli waliorudi toka katika uhamisho:

8ukoo wa Parosi: elfu mbili mia moja makumi saba na wawili;

9ukoo wa Sefatia: mia tatu makumi saba na wawili;

10ukoo wa Ara: mia sita makumi tano na wawili;

11ukoo wa Pahati-Moabu, ni kusema wazao wa Yesua na Yoabu: elfu mbili mia nane na kumi na wanane;

12ukoo wa Elamu: elfu moja mia mbili makumi tano na wane;

13ukoo wa Zatu: mia nane makumi ine na watano;

14ukoo wa Zakayi: mia saba na makumi sita;

15ukoo wa Binui: mia sita makumi ine na wanane;

16ukoo wa Bebayi: mia sita makumi mbili na wanane;

17ukoo wa Azgadi: elfu mbili mia tatu makumi mbili na wawili;

18ukoo wa Adonikamu: mia sita makumi sita na saba;

19ukoo wa Bigwayi: elfu mbili na makumi sita na saba;

20ukoo wa Adini: mia sita makumi tano na watano;

21ukoo wa Ateri (ambao vilevile unaitwa Hezekia): makumi kenda na wanane;

22ukoo wa Hasumu: mia tatu makumi mbili na wanane;

23ukoo wa Besayi: mia tatu makumi mbili na wane;

24ukoo wa Harifu: mia moja kumi na wawili;

25ukoo wa Gibeoni: makumi kenda na watano.

26Watu wa miji hii vilevile walirudi:

wa muji wa Betelehemu na Netofa: mia moja makumi nane na wanane;

27wa muji wa Anatoti: mia moja makumi mbili na wanane;

28wa muji wa Beti-Azimaweti: makumi ine na wawili;

29wa miji ya Kiriati-Yearimu, Kefira na Beroti: mia saba makumi ine na watatu;

30wa miji ya Rama na Geba: mia sita makumi mbili na mumoja;

31wa muji wa Mikimasi: mia moja makumi mbili na wawili;

32wa miji ya Beteli na Ai: mia moja makumi mbili na watatu;

33wa muji mwingine wa Nebo: makumi tano na wawili;

34wa muji mwingine wa Elamu: elfu moja mia mbili makumi tano na wane;

35wa muji wa Harimu: mia tatu na makumi mbili;

36wa muji wa Yeriko: mia tatu makumi ine na watano;

37wa miji ya Lodi, Hadidi na Ono: mia saba makumi mbili na mumoja;

38wa muji wa Sena: elfu tatu mia tisa na makumi tatu.

39Hii ndiyo hesabu ya makuhani waliorudi kutoka katika uhamisho:

makuhani wa ukoo wa Yedaya, waliokuwa wazao wa Yesua: mia tisa makumi saba na watatu;

40wa ukoo wa Imeri: elfu moja na makumi tano na wawili;

41wa ukoo wa Pashuri: elfu moja mia mbili makumi ine na saba;

42wa ukoo wa Harimu: elfu moja na kumi na saba.

43Walawi wa ukoo wa Yesua, ni kusema Kadimieli, wazao wa Hodavia waliorudi kutoka katika uhamisho walikuwa makumi saba na wane.

44Waimbaji: wazao wa Asafu walikuwa mia moja makumi ine na wanane.

45Walinzi wa milango walikuwa wazao wa:

Salumu, Ateri, Talmoni,

Akubu, Hatita, Sobayi.

Walikuwa mia moja makumi tatu na wanane.

46-56Ukoo za watumishi wa hekalu waliorudi kutoka katika uhamisho zilikuwa ukoo za:

Siha, Hasufa, Tabaoti,

Kerosi, Siaha, Padoni,

Lebana, Hagaba, Salmai,

Hanani, Gideli, Gahari,

Reaya, Resini, Nekoda,

Gazamu, Uza, Pasea,

Besayi, Munimu, Nefusesimu,

Bakibuki, Hakufa, Harihuri,

Basiliti, Mehida, Harsa,

Barkosi, Sisera, Tema,

Nezia, Hatifa.

57-59Ukoo za wazao wa watumishi wa mufalme Solomono waliorudi kutoka katika uhamisho zilikuwa ukoo za:

Sotayi, Sofereti, Perida,

Yala, Darkoni, Gideli,

Sefatia, Hatili,

Pokereti-Hazebaimu, Amoni.

60Watumishi wote wa hekalu na wazao wa watumishi wa Solomono, waliorudi kutoka katika uhamisho, walikuwa mia tatu makumi tisa na wawili.

61Watu walirudi kutoka miji hii:

Teli-Mela, Teli-Harsa,

Kerubu, Adoni, Imeri.

Lakini haikuwezekana kuhakikisha kwamba walikuwa wazao wa Waisraeli.

62Wao walikuwa wazao wa Delaya, Tobia na wa Nekoda, kwa jumla: watu mia sita makumi ine na wawili.

63Wazao wa ukoo hizi zinazofuata za makuhani vilevile walirudi: ukoo wa Hobaya, wa Hakosi na wa ukoo wa Barzilayi (aliyekuwa ameoa wabinti za Barzilayi, Mugileadi, naye akatwaa jina la ukoo ule.)

64Hao walitafuta kitabu cha vizazi vyao kati ya wengine walioandikwa katika kitabu cha ukumbusho za ukoo, lakini ukoo wao haukuonekana. Kwa hiyo hawakuruhusiwa kutiwa katika kazi ya ukuhani maana walihesabiwa kuwa wachafu.

65Mutawala akawaambia kwamba hawaruhusiwi kushiriki kwa chakula kitakatifu sana, mpaka kuhani anayeweza kutumia Urimu na Tumimu afike.

66-68Hii ni jumla ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho, pamoja na watumishi na nyama wao.

Waisraeli: elfu makumi ine na mbili mia tatu na makumi sita;

Watumishi wanaume na wanawake: elfu saba mia tatu makumi tatu na saba;

Waimbaji wanaume na wanawake: mia mbili makumi ine na watano;

Ngamia: mia ine makumi tatu na watano;

Punda: elfu sita mia saba na makumi mbili.

69Wakubwa wamoja wa ukoo walichangia kazi ya ujenzi. Mutawala wa jimbo alitoa kilo nane za zahabu, mabeseni makumi tano, nguo mia tano na makumi tatu ya makuhani.

70Wakubwa wa ukoo walitoa kilo mia moja makumi sita na nane za zahabu, na kilo elfu moja mia mbili na makumi tano za feza.

71Matoleo ya watu wengine wote yalikuwa kilo mia moja makumi sita na nane za zahabu, kilo mia moja makumi ine za feza na nguo za makuhani makumi sita na saba.

72Basi, makuhani, Walawi, walinzi wa hekalu, waimbaji, pamoja na watu wengine, watumishi wa hekalu na watu wote wa Israeli, wakaishi katika miji yao.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help