1Kwa kutumia sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu walifuma nguo za kuvaa wakati wa kutumika katika Pahali Patakatifu. Walimushonea Haruni nguo takatifu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
2Wakatengeneza kizibao kwa nyuzi za zahabu, kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kwa kitani safi iliyosokotwa.
3Wakafua zahabu na kuikata katika nyuzi nyembamba kwa kuzifuma pamoja na sufu ya rangi ya samawi, ya zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa kwa ufundi.
4Kizibao hicho kilivaliwa kwa kamba mbili juu ya mabega zilizoshonewa kwenye incha zake mbili.
5Mukaba uliofumwa kwa ufundi juu yake kwa kuifunga ulikuwa kitu kimoja na kizibao hicho, na ulitengenezwa kwa vitu hivyohivyo: zahabu, sufu ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
6Kisha wakatayarisha mawe ya sardoniki na kuyapanga katika kingo za zahabu. Nayo yalichorwa, kama vile mutu anavyochora muhuri, majina kumi na mawili ya wana wa Israeli.
7Wakaweka mawe yale juu ya mikaba ya mabega za kila kizibao kuwa ukumbusho wa makabila kumi na mawili ya Israeli, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Kifuko cha kifua(Kut 28.15-30)8Wafundi walitengeneza kifuko cha kifua kama vile walivyotengeneza kile kizibao, kwa zahabu, kwa sufu ya rangi ya samawi, ya zambarau na ya nyekundu, na kwa kitani safi iliyosokotwa.
9Kifuko hicho kilikuwa cha muraba, sentimetre makumi mbili na mbili kwa sentimetre makumi mbili na mbili nacho kilikunjwa.
10Kifuko hicho kilipambwa kwa mistari mine ya mawe ya bei kali. Mustari wa kwanza ulikuwa wa akiki, topazi na almasi nyekundu.
11Mustari wa pili ulikuwa wa zumaridi, yakuti-samawi na almasi.
12Mustari wa tatu ulikuwa wa yasinto, akiki nyekundu na ametisto.
13Mustari wa ine ulikuwa wa zabarajadi, shohamu na yaspi. Yote yalifungwa ndani ya kingo za zahabu.
14Basi, kulikuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa juu yake majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Yalikuwa yamechorwa kama vile wanavyochora muhuri, juu ya kila moja kulichorwa jina kwa ukumbusho wa makabila kumi na mawili.
15Walitengenezea kile kifuko cha kifua mikufu ya zahabu safi.
16Wakatengeneza kingo mbili za zahabu safi na pete mbili za zahabu, na kutia pete hizo kwenye incha mbili za juu za kifuko hicho.
17Mikufu hiyo miwili ya zahabu wakaifunga kwenye pete hizo za kifuko cha kifua.
18Zile incha mbili za mikufu ya zahabu wakazitia kwenye zile kingo mbili wakazishikamanisha na vile vipande viwili vya mabega vya kizibao, upande wa mbele.
19Wakatengeneza pete mbili za zahabu, wakazitia kwenye incha mbili za chini upande wa ndani wa kifuko hicho cha kifua karibu na kizibao.
20Wakatengeneza pete zingine mbili za zahabu na kuzitia mbele katika incha za chini za vipande vya kizibao, pahali kinapoungana na ule mukaba uliofumwa kwa ufundi.
21Wakafunga kifuko cha kifua kwenye kizibao kwa kufunganisha pete zake na kizibao kwa kamba ya rangi ya samawi, kusudi kifuko hicho kisiregee lakini kiikalie ule mukaba uliofumwa kwa ufundi, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Nguo zingine za kikuhani(Kut 28.31-43)22Akatengeneza kanzu ya kuvaa ndani ya kizibao ya rangi ya samawi.
23Koti hilo lilikuwa na nafasi ya kupitishia kichwa katikati, nalo lilizungushiwa utepe uliofumwa kusudi isichanike.
24Kwenye upindo wa chini wa kanzu walifuma mapambo ya makomamanga ya rangi ya samawi, ya zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa.
25Kisha walitengeneza kengele za zahabu na kisha kila komamanga walitia kengele kwenye upindo wa koti.
26Hivyo, kengele na komamanga vilifuatana kuzunguka upindo wa koti hilo, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
27Kisha wakawafumia Haruni na wana wake vizibao vya kitani safi,
28kitambaa cha kitani safi, kofia za kitani safi, makapitula za kitani safi iliyosokotwa,
29na mikaba ya kitani safi iliyosokotwa kwa sufu ya rangi ya samawi, ya zambarau na nyekundu na kupambwa vizuri, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
30Kisha wakatengeneza pambo la zahabu safi kwa ajili ya taji takatifu na kuchora juu yake kama vile wanavyochora muhuri: Takatifu kwa Yawe.
31Kisha wakalifunga mbele ya kile kitambaa kwa mukaba wa rangi ya samawi, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Kukamilika kwa kazi(Kut 35.10-19)32Basi, kazi yote ya hema la mukutano ikamalizika. Waisraeli walifanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
33Wakamuletea Musa hema takatifu pamoja na vyombo vyake vyote, vifungio vyake, mbao zake, miti yake, nguzo zake na vikalio vyake;
34kifuniko cha ngozi za kondoo dume na mbuzi kilichotiwa rangi nyekundu, pazia la Pahali Patakatifu,
35Sanduku la Agano, miti yake na kiti cha rehema;
36meza na vyombo vyake vyote, mikate iliyotolewa kwa Mungu;
37kinara cha taa cha zahabu safi, taa zake, vyombo vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa hizo;
38mazabahu ya zahabu; mafuta ya kupakaa, ubani wenye harufu nzuri, na pazia la mulango wa hema;
39mazabahu ya shaba na wavu wake wa shaba, miti yake na vyombo vyake vyote; bakuli, birika na tako lake;
40mapazia ya upango, nguzo zake na vikalio vyake; pazia la mulango wa upango, kamba zake na misumari yake; vyombo vyote vilivyohitajika katika kazi ya hema takatifu, ni kusema hema la mukutano;
41na nguo zote zilizofumwa vizuri kabisa kwa ajili ya kazi ya Pahali Patakatifu, ni kusema nguo takatifu za kuhani Haruni, na za wana wake kwa ajili ya kazi za ukuhani.
42Waisraeli walifanya kila kitu kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
43Musa akachunguza kila kitu, akaona kwamba walikuwa wamefanya kila kitu kama vile Yawe alivyoamuru. Hivyo Musa akawabariki.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.