Zaburi 128 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Baraka ya wenye kumutii Mungu

1Wimbo wa safari za kidini.

Heri wote wanaomwabudu Yawe,

wanaoishi kufuatana na amri zake.

2Utapata matunda ya jasho lako,

utafurahi na kupata uheri.

3Muke wako atakuwa kama muzabibu wenye matunda mengi;

watoto wako kama vichipukizi vya muzeituni kuzunguka meza yako.

4Kweli, hivi ndivyo atakavyobarikiwa

mutu anayemwabudu Yawe.

5Yawe akubariki kutokea Sayuni!

Uone uheri wa Yerusalema,

siku zote za maisha yako.

6Uishi na hata uwaone wajukuu wako!

Amani ikuwe na Israeli!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help