1“Mutu akipatikana ameuawa katika mbuga katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa kuwa urizi wenu, nanyi hamujui ni nani aliyemwua,
2wazee na waamuzi wenu watajitokeza na kupima umbali wa kutoka pahali maiti inapokuwa mpaka kwenye miji ya karibu.
3Kisha, wazee wa muji ule unaokuwa karibu zaidi na ile maiti watatwaa mwana-ngombe ambaye hajatumiwa kufanya kazi yoyote wala kutiwa nira.
4Nao watamuteremusha mwana-ngombe katika bonde kwenye kijito ambacho hakikauki, na bonde hilo halilimwi au kupandwa. Huko watamuvunja huyo mwana-ngombe shingo.
5Nao makuhani wa ukoo wa Lawi sharti wakuwe pale. Yawe, Mungu wenu, aliwachagua wamutumikie na kubariki kwa jina lake. Wao vilevile ndio wenye mamlaka ya kuamua magomvi na maneno juu ya kuumizana.
6Yule mwana-ngombe atakapovunjwa shingo, wazee wote wa muji huo unaokuwa karibu na mutu huyo aliyeuawa, watanawa mikono yao kwa maji juu ya mwana-ngombe
7na kusema: ‘Hatuna kosa juu ya kifo hiki, wala hatumujui aliyemwua.
8Ee Yawe, uwasamehe watu wako wa Israeli ambao umewakomboa, usiwawekee watu wako Israeli kosa la mauaji ya mutu asiyekuwa na kosa, lakini uwasamehe kosa lile.’
9Hivyo damu hiyo iliyomwangwa haitakuwa tena sababu ya hukumu kwenu, maana mumefanya yale Yawe aliyotaka mufanye.
10“Mukienda kupigana vita na adui, naye Yawe akiwapa ushindi, na kuteka vitu,
11kama mumoja wenu akiona kati ya vitu vilivyotekwa mwanamuke muzuri, akimutamani na kutaka kumwoa,
12basi, anaweza kumupeleka kwake. Yule mwanamuke atanyoa kichwa chake na kukata kucha zake,
13na kubadilisha nguo zake za kitumwa. Atakaa muda wa mwezi muzima kwa kumwomboleza baba yake na mama yake. Kisha mwanaume huyo anaweza kumwoa.
14Kama kisha hapendezwi naye, atamwacha aende anakotaka. Mwanaume huyo hatamwuzisha kwa kupata feza, wala hatamutendea kama vile mutumwa kwa sababu amemunyenyekeza.
15“Ikiwa mwanaume fulani ana wake wawili naye anamupenda mumoja kuliko mwingine, nao wanawake hao wamemuzalia watoto wanaume, na mutoto wa kwanza kuzaliwa ni wa yule mama asiyemupenda,
16ikifika siku ya kuwapa hao wanawake urizi, huyo baba haruhusiwi kumutendea mutoto wa yule muke anayemupenda kama kwamba ni mutoto muzaliwa wa kwanza, pahali pa yule mutoto wa mama asiyependwa ambaye ndiye anayekuwa muzaliwa wa kwanza.
17Anapaswa kukubali yule muzaliwa wa kwanza, mutoto wa yule mwanamuke asiyependwa, na kumupa haki yake: sehemu ya mali zake mara mbili.
18“Kama mutu ana mutoto mwenye kiburi na mwasi, asiyemutii baba yake au mama yake ingawa wanamwazibu,
19basi, mama na baba ya huyo mutoto watamutwaa kumupeleka kwa wazee muji kwenye tribinali.
20Wazazi hao watawaambia wazee wa muji: ‘Mutoto wetu ni mwenye kiburi na mwasi, hataki kutusikiliza, ni mulafi na mulevi’.
21Hapo watu wa muji huo watamupiga mutoto huyo mawe mpaka akufe. Ndivyo mutakavyokomesha ubaya huo kati yenu. Kila mutu katika Israeli atasikia tukio hilo na kuogopa.
Sheria mbalimbali22“Kama mutu amefanya kosa linalomupasa auawe na akiuawa kwa kutundikwa juu ya muti,
23maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.