1Yawe akamwambia Musa na Haruni:
2Uwaambie Waisraeli hivi: Mwanaume yeyote akitokwa na usaha, usaha huo unamufanya kuwa muchafu.
3Na hii ndiyo sheria juu ya uchafu huo: muda wote anapotokwa na usaha au usaha unapokuwa umezuiwa ndani yake, mutu yule ni muchafu.
4Kitanda chochote atakacholalia au atakachoikalia, kitakuwa kichafu.
5Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha mutu yule anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
6Mutu yeyote atakayeikalia kitu chochote mutu huyu mwenye kutokwa na usaha alichoikalia, anapaswa kufua nguo na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
7Mutu yeyote atakayegusa mutu anayetokwa na usaha, anapaswa kufua nguo zake na kuoga; naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.
8Mutu yeyote akitemewa mate na mutu anayetokwa usaha, yule aliyetemewa mate anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
9Tandiko lolote la nyama ambalo mutu anayetokwa na usaha aliikalia litakuwa chafu.
10Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mutu huyu alichoikalia atakuwa muchafu mpaka magaribi. Mutu yeyote anayebeba kitu chochote kilichokuwa cha mutu huyu anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
11Mutu yeyote anayetokwa na usaha akimugusa mutu bila kusafisha kwanza mikono yake na kuoga, aliyeguswa atakuwa muchafu mpaka magaribi.
12Chombo chochote cha udongo kilichoguswa na mutu anayetokwa na usaha kinapaswa kuvunjwa. Lakini chombo chochote cha mbao kitasafishwa kwa maji.
13Mwanaume yeyote anayetokwa na usaha akiponywa ugonjwa wake, mutu yule anapaswa kungoja siku saba mbele ya kuondolewa uchafu wake. Atafua nguo zake na kuoga kwa maji ya muto, naye atakuwa safi.
14Siku ya nane, anapaswa kuleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa mbele ya Yawe kwenye mulango wa hema la mukutano na kumupatia kuhani.
15Kuhani atatoa hao, mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kuhani atamufanyia mutu huyu ibada ya upatanisho mbele ya Yawe na kumwondolea uchafu wake wa kutokwa na usaha.
16Mwanaume yeyote akitokwa na mbegu za uzazi, anapaswa kuoga mwili muzima kwa maji, naye atakuwa muchafu mpaka magaribi.
17Nguo yoyote iliyodondokewa mbegu za uzazi au ngozi yoyote iliyoguswa na mbegu zile inapaswa kusafishwa kwa maji na itakuwa chafu mpaka magaribi.
18Kama mwanaume akilala na mwanamuke na kutokwa na mbegu za uzazi, basi, ni lazima wote wawili waoge kwa maji, nao watakuwa wachafu mpaka magaribi.
19Mwanamuke yeyote anapokuwa na ugonjwa wa mwezi, atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba. Mutu yeyote atakayemugusa mwanamuke yule atakuwa muchafu mpaka magaribi.
20Kitu chochote anacholalia au kuikalia wakati wa kutengwa kwake kitakuwa kichafu.
21Mutu yeyote atakayegusa kitanda cha huyo mwanamuke anapaswa kufua nguo zake na kuoga kwa maji. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
22Mutu yeyote atakayegusa kitu chochote mwanamuke huyo anachoikalia anapaswa kufua nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa muchafu mupaka magaribi.
23Mwanaume yeyote atakayegusa kitu chochote mwanamuke yule alicholalia au kuikalia, atakuwa muchafu mpaka magaribi.
24Kama mwanaume akilala na mwanamuke huyo na damu ya huyo mwanamuke ikimudondokea huyo mwanaume, basi, mwanaume huyo atakuwa muchafu kwa muda wa siku saba. Kitanda chochote huyu mwanaume atakacholalia kitakuwa kichafu.
25Kama mwanamuke anatokwa na damu kwa muda wa siku nyingi kuliko vile inavyokuwa kawaida au anatokwa damu wakati usiokuwa wa kawaida yake ya kutokwa damu, basi, ataendelea kuwa muchafu muda wote damu inapomutoka.
26Kitanda chochote anacholalia wakati ule au kiti chochote anachoikalia, kitakuwa kichafu sawa kama wakati wake wa kutengwa.
27Mutu yeyote atakayegusa vitu hivyo, atakuwa muchafu na anapaswa kufua nguo zake na kuoga. Atakuwa muchafu mpaka magaribi.
28Nyuma ya kukauka damu yake mwanamuke huyo atangoja bado siku saba kwa kuwa safi, na nyuma ya muda ule atakuwa safi.
29Siku ya nane atatwaa hua wawili au vitoto viwili vya njiwa na kumuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano.
30Kuhani atatoa mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Hivyo kuhani atamufanyia huyo mwanamuke ibada ya upatanisho mbele ya Yawe na kumwondolea uchafu wake wa kutokwa damu.
31Ndivyo mutakavyotenga Waisraeli na uchafu wao, kusudi wasikufe katika uchafu wao juu ya kuchafua hema langu linalokuwa kati yao.
32Hiyo ndiyo sheria juu ya mwanaume anayetokwa na usaha na anayetokwa na mbegu za uzazi na kuwa muchafu.
33Sheria hiyo inaelekea vilevile mwanamuke anayetokwa damu na kuwa muchafu. Sheria hiyo inaelekea mwanaume au mwanamuke yeyote anayetokwa na chochote na vilevile inaelekea mwanaume anayelala na mwanamuke ambaye ni muchafu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.