1Heshima anayopewa mupumbafu haifai. Ni kama teluji ya wakati wa kipwa, au mvua ya wakati wa mavuno.
2Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.
3Kiboko ni kwa farasi, lijamu ni kwa punda, na fimbo ni kwa mugongo wa mupumbafu.
4Usimujibu mupumbafu kipumbafu, kusudi usifanane naye.
5Umujibu mupumbafu kama kufuatana na upumbafu wake, kusudi asijione kuwa mwenye hekima zaidi.
6Kutuma ujumbe kwa mukono wa mupumbafu ni kama kujikata miguu au kujitafutia mateso.
7Mezali katika midomo ya mupumbafu ni kama miguu ya kiwete inayoninginia.
8Kumupa mupumbafu heshima ni kama kufunga jiwe kwenye mujeledi.
9Mezali katika kinywa cha mupumbafu ni kama tawi lenye miiba katika mukono wa mulevi.
10Mutu anayemulipa mupumbafu au mulevi kusudi amutumikie, ni kama mupiga upinde anayeumiza kila mutu.
11Mupumbafu anayerudiliarudilia upumbafu wake ni kama imbwa anayekula matapiko yake.
12Unamwona mutu anayejiona kuwa mwenye hekima? Afazali kumutumainia mupumbafu kuliko yule.
13Muvivu anasema: “Kuna simba kali inje. Kuna simba katika njia.”
14Kama vile mulango unavyozunguka kwenye vyuma vya kuukamatia, ndivyo muvivu anavyogeuka juu ya kitanda chake.
15Muvivu anatia mukono wake katika sahani, lakini anachoka kwa kuuinua mpaka kwenye mudomo.
16Muvivu anajiona kuwa mwenye hekima kuliko watu saba wanaoweza kujibu kwa akili.
17Anayejiingiza katika ugomvi usiomwelekea, ni kama mutu anayeshika masikio ya imbwa anayepita.
18Kama vile mwenda-wazimu anavyotupa mienge ya moto, mishale, na kifo,
19ndivyo mutu ambaye anadanganya jirani, kisha anasema: “Nilikuwa ninafanya muzaha tu!”
20Bila kuni, moto unazimika; bila mwenye kuchochea, ugomvi unamalizika.
21Kama vile makaa au kuni vinachochea moto, ndivyo mugomvi anachochea ugomvi.
22Maneno ya muchongeaji ni kama chakula kitamu; yanashuka mpaka ndani kabisa ya tumbo.
23Kama vile rangi yenye kungaa iliyopakwa juu ya chungu cha udongo, ndivyo maneno matamu yenye nia mbaya yanavyokuwa.
24Mwenye chuki anaficha chuki yake kwa maneno mazuri, lakini uovu unajaa ndani ya moyo wake.
25Akisema maneno mazuri usimwaminie. Ndani ya moyo wake kuna machukizo mengi.
26Anaweza kuficha chuki yake, lakini nia zake mbaya zitajulikana kwa wote.
27Anayechimbia mwenzake shimo, anatumbukia ndani mwenyewe; anayewaporomoshea wengine jiwe, litamurudilia mwenyewe.
28Anayesema uongo anachukia wale anaowaumiza, naye anayebembeleza analeta maangamizi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.