1Wimbo wa safari za kidini.
Ninainua macho kwako, ee Yawe,
wewe unayeikaa huko juu mbinguni!
2Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao,
kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake,
ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe,
ee Yawe, Mungu wetu,
mpaka hapo utakapotuonea huruma.
3Utuhurumie, ee Yawe, utuhurumie,
maana tumezarauliwa kupita kipimo.
4Tumeshiba muda murefu mazarau ya watajiri,
nayo masimango ya wenye kiburi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.