Maombolezo 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Yerusalema kisha kuangamizwa

1Namna gani zahabu yetu ilivyochakaa,

zahabu safi kabisa ilivyobadilika!

Mawe ya bei kali yamesambazwa

kwa barabara zote.

2Watoto wa Sayuni waliosifiwa sana,

waliokuwa na bei kama zahabu safi,

namna gani sasa wamekuwa kama vyombo vya udongo,

kazi ya mikono ya mufinyanzi!

3Hata mbweha wanatoa maziwa,

na kuwanyonyesha watoto wao;

lakini watu wangu wamekuwa wabaya,

wanafanya kama mbuni katika jangwa.

4Midomo ya watoto wachanga imekauka kwa kiu,

watoto wanaomba chakula, lakini hakuna anayewapa.

5Wale waliokula vyakula vinono

wanakufa na njaa katika barabara.

Waliolelewa na kuvalishwa namna ya kifalme

wanafukua kwa mikono kwenye yalala.

6Kosa la watu wangu lilikuwa kubwa

kuliko zambi za watu wa Sodoma,

muji ambao uliteketezwa kwa rafla

bila kuwa na muda wa kunyoosha mukono.

7Vijana wa Sayuni walikuwa safi kuliko teluji,

walikuwa weupe kuliko maziwa.

Miili yao ilikuwa myekundu kuliko mawe ya matumbawe,

uso wao kama jiwe la rangi ya samawi.

8Sasa sura zao ni nyeusi kuliko makaa,

wanapita katika barabara bila kujulikana;

ngozi yao imebanana na mifupa yao,

imekauka, imekuwa kama kuni.

9Afazali waliouawa kwa upanga

kuliko waliokufa kwa njaa,

ambao walikufa polepole

kwa kukosa mazao ya shamba.

10Wamama ambao wanakuwa na huruma kubwa,

waliwapika watoto wao wenyewe,

wakawafanya kuwa chakula chao,

wakati watu wangu walipoangamizwa.

11Yawe ameonyesha kabisa kasirani yake,

aliimwanga hasira yake kali,

aliwasha moto huko katika Sayuni

ambao uliteketeza misingi yake.

12Wafalme katika dunia hawakuamini

wala wakaaji wowote wa ulimwengu,

kwamba mwangamizaji na adui

wangeweza kuingia katika milango ya Yerusalema.

13Ni kwa sababu ya zambi za manabii wake

na makosa ya makuhani wake,

ambao walimwanga damu ya watu wa haki katika muji wake.

14Walitangatanga katika barabara kama vipofu,

walikuwa wamejichafua kwa damu,

hata mutu yeyote hangeweza kugusa nguo zao.

15Watu waliwapigia kelele wakisema:

Mutoke, enyi munaokuwa wachafu!

Mutoke! Mutoke! Musiguse kitu chochote.

Hivyo wakakuwa wakimbizi na kutangatanga;

watu wa mataifa walisema:

Hawa hawatakaribishwa kukaa kwetu!

16Yawe mwenyewe aliwatawanya,

wala hatawajali tena.

Makuhani hawaheshimiwi tena,

wazee hawapendelewi tena.

17Tulichoka kukaa macho kungojea musaada;

tulikesha na kungojea kwa hamu

taifa ambalo halikuweza kutuokoa.

18Watu walifuatilia hatua zetu,

tukashindwa kupita katika barabara zetu.

Mwisho wetu ulikaribia,

siku zetu zilitimia,

mwisho wetu ulifika.

19Waliotufuatilia walikuwa wepesi kuliko tai,

walitukimbiza kwenye milima

walituvizia katika jangwa.

20Walimunasa yule ambaye maisha yetu yalimutegemea,

yule mufalme aliyechaguliwa na Yawe

yule ambaye tulisema juu yake: Chini ya ulinzi wake

tutaishi kati ya mataifa.

21Wakaaji wa Edomu, ile inchi ya Uzi,

mushangilie na kufurahi kwa sasa.

Lakini kikombe hiki cha azabu kitawafikia vilevile.

Mutakikunywa na kulewa,

hata mutavaa uchi!

22Azabu ya uovu wako, ewe Sayuni imekamilika;

Yawe hatawaacha zaidi katika uhamisho.

Lakini ninyi Waedomu atawaazibu kwa uovu wenu,

atazifichua zambi zenu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help