1Wakati huo, Wafilistini walikutana pamoja, wapigane na Waisraeli. Waisraeli walipiga kambi yao kule Ebeni-Ezeri, na Wafilistini wakapiga kambi yao kule Afeki.
2Wafilistini waliwashambulia Waisraeli, na nyuma ya mapigano makali, Waisraeli walishindwa. Waisraeli elfu ine waliuawa kwenye uwanja wa vita.
3Waaskari walioponyoka walipofika kwenye kambi, wazee wa Israeli walisema: “Kwa nini Yawe amewaacha Wafilistini watushinde leo? Tuende tulilete Sanduku la Agano la Yawe kutoka Shilo, kusudi aweze kwenda nasi katika vita na kutuokoa kutoka waadui zetu.”
4Kwa hiyo, walituma watumishi kule Shilo, nao wakalileta Sanduku la Agano la Yawe wa majeshi ambaye anatawala juu ya makerubi. Wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi walikuja pamoja na lile Sanduku la Agano la Mungu.
5Sanduku la Agano la Yawe lilipofika katika kambi Waisraeli wote walishangilia kwa furaha, hata inchi yote ikatikisika.
6Wafilistini waliposikia sauti hiyo ya furaha walisema: “Kelele hiyo yote katika kambi ya Waebrania ina maana gani?” Walipojua kwamba Sanduku la Agano la Yawe lilikuwa limefika katika kambi ya Waisraeli,
7Wafilistini waliogopa. Wakasema: “Bila shaka, miungu imefika katika kambi yao! Ole wetu! Jambo kama hili halijatokea tangia zamani.
8Ole wetu! Ni nani atakayeweza kutuokoa kutokana na miungu hiyo yenye nguvu? Hiyo ni miungu iliyowaua Wamisri kwa kila aina ya mapigo katika jangwa.
9Sasa, enyi Wafilistini, mujipe moyo. Mukuwe hodari kusudi musipate kuwa watumwa wa Waebrania kama wao walivyokuwa watumwa wetu. Mukuwe hodari kama wanaume na kupigana.”
10Wafilistini walipiga vita, na Waisraeli walishindwa na kukimbia kila mutu kwake. Siku hiyo kulikuwa mauaji makubwa maana waaskari wa miguu elfu makumi tatu wa Israeli waliuawa.
11Sanduku la Agano la Mungu lilitekwa, na wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, wakauawa.
Kifo cha Eli12Siku hiyohiyo, mutu mumoja wa kabila la Benjamina alikimbia kutoka mustari wa mbele wa mapigano mpaka Shilo nazo nguo zake zikiwa zimechanika na akiwa na mavumbi kwenye kichwa.
13Eli, akiwa na wasiwasi ndani ya moyo juu ya Sanduku la Mungu, alikuwa ameikaa kwenye kiti chake, pembeni ya barabara akiangalia. Yule mutu alipofika katika muji na kueleza habari hizo, muji muzima ulilia kwa sauti.
14Eli aliposikia sauti ya kilio, akauliza: “Kelele hizo ni za nini?” Yule mutu akaenda haraka kwa Eli kwa kumupa habari hizo.
15Wakati huo, Eli alikuwa na umri wa miaka makumi kenda na nane na macho yake yalikuwa yamepofuka.
16Yule mutu akamwambia Eli: “Mimi nimetoka kwenye vita; nimekimbia kutoka katika vita leo.”
Eli akamwuliza: “Mwana wangu, mambo yalikuwa namna gani kule?”
17Yule aliyeleta habari akasema: “Waisraeli wamewakimbia Wafilistini. Kumekuwa mauaji makubwa kati ya Waisraeli. Zaidi ya yote, wana wako wote wawili, Hofuni na Finehasi, wameuawa, na Sanduku la Agano la Mungu limetekwa.”
18Huyo mutu alipotaja tu Sanduku la Mungu, Eli alianguka machali kutoka kwenye kiti chake pembeni ya mulango. Eli alipoanguka hivyo, shingo yake ilivunjika maana alikuwa muzee na munene, naye akakufa. Eli alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka makumi ine.
Kifo cha mujane wa Finehasi19Tena ilitokea kwamba, mukwe wa Eli, ni kusema muke wa Finehasi, kwa wakati ule alikuwa na mimba, na muda wake wa kuzaa ulikuwa umekaribia. Aliposikia kwamba Sanduku la Agano la Mungu limetekwa na kwamba baba mukwe wake, hata na mume wake wamekufa, mara moja akapata maumivu ya kuzaa. Kwa hiyo akachutama na kuzaa.
20Basi, kwa sababu alikuwa karibu ya kufa, wanawake waliokuwa wanamuzalisha walimwambia: “Usiogope, maana umezaa mutoto mwanaume.” Lakini yeye hakujibu neno, wala hakuwasikiliza.
21Naye akamwita mutoto wake Ikabodi, maana alisema: “Utukufu wa Mungu umeondolewa kwa Waisraeli”, akiwa na maana kwamba Sanduku la Agano lilikuwa limetekwa, tena baba mukwe wake na mume wake, wote walikufa.
22Akasema: “Utukufu wa Mungu umeondolewa kwa Waisraeli maana Sanduku la Agano la Yawe limetekwa.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.