1Hili ni neno la Yawe lililomufikia Yoeli mwana wa Petueli.
Watu wanaomboleza juu ya mimea2Musikilize kitu hiki, enyi wazee;
mutege sikio, ninyi wakaaji wote wa Yuda!
Jambo kama hili limekwisha kutokea katika maisha yenu,
au nyakati za babu zenu?
3Muwaelezee watoto wenu jambo hili,
nao wawaelezee watoto wao,
na watoto wao wakielezee kizazi kinachofuata.
4Nzige, makundi kwa makundi, wameishambulia mimea;
kilichoachwa na nzige kimekuliwa na tunutu,
kilichoachwa na tunutu kimekuliwa na parare,
kilichoachwa na parare kimeliwa na panzi.
5Enyi walevi, muamuke na kulia;
enyi walevi wa divai, mulalamike;
zabibu zote za kutengeneza divai mupya zimeharibiwa.
6Jeshi la nzige limeishambulia inchi yetu;
lina nguvu na ni kubwa ajabu;
meno yake ni kama ya simba,
na mataya yake ni kama ya simba dike.
7Limeiharibu mizabibu yetu,
na kuitafuna mitini yetu.
Limeyabandua maganda yake na kuyatupa chini,
na matawi yake yameachwa meupe.
8Mulie kama vile binti aliyevaa gunia
akiombolezea kifo cha muchumba wake.
9Sadaka za vyakula na za kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Yawe.
Makuhani, watumishi wa Yawe, wanaomboleza.
10Mashamba yamebaki matupu.
Inchi inaomboleza,
maana ngano imeharibiwa,
divai imetoweka,
mafuta yamekosekana.
11Muomboleze, enyi walimaji;
mulalamike, enyi watunza mizabibu.
Ngano na shayiri zimeharibika,
mavuno yote katika shamba yameangamia.
12Mizabibu imenyauka,
mitini imekauka,
miti yote ya matunda imekauka.
Furaha imetoweka kati ya watu.
13Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza,
mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu.
Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha!
Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.
14Mutoe amri watu wafunge kula chakula;
muwaalike watu kuja kwa mukutano wa kidini.
Mukusanye wazee na wakaaji wote wa inchi,
katika nyumba ya Yawe, Mungu wenu,
na mule mumulilie Yawe.
15Ole kwetu kwa ile siku ya Yawe,
siku hiyo ya Yawe inakaribia;
inakuja pamoja na maangamizi,
kutoka kwa Mungu Mukubwa.
16Mazao yetu yameharibiwa mbele ya macho yetu.
Furaha na kicheko vimetoweka katika nyumba ya Mungu wetu.
17Mbegu zinaoza ndani ya udongo;
gala zimebaki bila kitu,
vibanda vya kuwekea mavuno vimebomoka,
kwa maana hakuna tena ngano.
18Angalia jinsi nyama wanavyolia kwa huzuni!
Makundi ya ngombe yanahangaika,
kwa sababu yamekosa malisho;
hata makundi ya kondoo yanateswa.
19Ninakulilia wewe, ee Yawe,
moto umemaliza malisho katika mbuga,
ndimi za moto zimeteketeza miti katika mashamba.
20Hata nyama wa pori wanakulilia wewe,
maana, vijito vya maji vimekauka,
moto umemaliza malisho katika mbuga.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.