Kutoka 24 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Agano linahakikishwa

1Yawe akamwambia Musa: Mukuje kwangu, wewe Haruni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee makumi saba wa Israeli, muniabudu kwa mbali.

2Wewe Musa peke yako ndiwe utakayenikaribia, lakini wengine wasikuje karibu na Waisraeli wasipande juu ya mulima pamoja nawe.

3Basi, Musa akaenda na kuwaambia watu wote maneno na maagizo yote Yawe aliyomwambia. Watu wote wakajibu kwa sauti moja: Mambo yote Yawe aliyosema, tutayafanya.

4Musa akaandika maagizo yote ambayo Yawe alimupa. Kisha akaamuka asubui mapema, akajenga mazabahu chini ya mulima na kusimamisha nguzo kumi na mbili kulingana na hesabu ya makabila kumi na mbili ya Israeli.

5Kisha akatuma vijana wa watu wa Israeli wamutolee Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na kumuchinjia sadaka za amani za ngombe.

6Musa akachota nusu ya damu ya nyama wale na kuiweka katika mabeseni na nusu ingine akainyunyiza juu ya mazabahu ile.

7Kisha akatwaa kitabu cha agano la Yawe, akakisoma mbele ya watu, nao wakasema: Yale yote Yawe aliyoyasema tutayafanya, nasi tutakuwa watiifu.

8Musa akatwaa ile damu na kuwanyunyizia watu, akisema: Hii ndiyo damu ya agano ambalo Yawe amefanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.

9Kisha Musa, Haruni, Nadabu na Abihu na wazee makumi saba wa Israeli wakapanda juu ya mulima,

10wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, kikiwa safi kama mbingu inayoangaa.

11Na Mungu hakuwazuru wale viongozi wa watu wa Israeli. Walimwona Mungu, wakakula na kunywa.

Musa juu ya mulima Sinai

12Yawe akamwambia Musa: Kuja kwangu juu kwenye mulima, ungoje kule. Mimi nitakupa vibao vya mawe vyenye sheria na amri nilizoandika kwa ajili ya kuwafundisha Waisraeli.

13Basi, Musa akaondoka pamoja na Yoshua, mutumishi wake, akaenda kwenye mulima wa Mungu.

14Musa aliwaambia wale wazee: Mutungojee hapa mpaka tutakapowarudilia. Haruni na Huri wako pamoja nanyi. Yeyote anayekuwa na tatizo awaendee wao.

15Basi, Musa akaenda kwenye mulima na wingu likafunika mulima.

16Utukufu wa Yawe ukatua juu ya mulima Sinai na wingu likafunika mulima kwa muda wa siku sita. Siku ya saba Mungu akamwita Musa kutoka katikati ya lile wingu.

17Utukufu wa Yawe ukaonekana mbele ya macho ya watu wa Israeli kama moto unaowaka juu ya mulima.

18Musa akaingia ndani ya lile wingu, akapanda kwenye mulima. Alikaa kule kwa muda wa siku makumi ine, muchana na usiku.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help