Isaya 23 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maangamizi ya Tiro na Sidona

1Ujumbe wa Mungu juu ya Tiro.

Muomboleze, enyi mashua makubwa za kutoka Tarsisi.

Kivuko na muji wenu vimeharibiwa.

Mutapokea habari hizo mutakaporudia kutoka Kipuro.

2Munyamaze kwa mushangao, enyi wakaaji wa visanga,

mutulie enyi wachuuzi wa Sidona.

Wajumbe wenu walipita katika bahari kubwakubwa,

3walisafiri katika bahari nyingi.

Mapato yenu yalikuwa ngano ya Misri,

mukaweza kufanya biashara na mataifa.

4Umefezeheka, ewe Sidona,

muji wenye upango kandokando ya bahari!

Bahari yenyewe inatangaza:

Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa,

wala sijazaa;

sikulea vijana wanaume,

wala kukomalisha wabinti!

5Habari zitakapoifikia Misri

kwamba Tiro imeangamizwa,

Wamisri watafazaika sana.

6Muomboleze enyi wenyeji wa Foinike!

Mujaribu kukimbilia Tarsisi.

7Basi, huu ndio muji wa furaha wa Tiro,

muji ambao ulijengwa zamani za kale,

ambao wakaaji wake walikwenda kurizi inchi za mbali?

8Ni nani aliyepanga mambo haya juu ya Tiro,

muji uliosimika wafalme,

wachuuzi wake walikuwa wakubwa,

wakaheshimiwa katika dunia yote?

9Ni Yawe wa majeshi!

Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote.

Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao

na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.

10Mulime sasa udongo wenu, enyi wakaaji wa Tarsisi;

maana hamuna tena kivuko kwa ajili ya mashua kubwa.

11Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari

amezitetemesha falme;

ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.

12Alisema: Ewe binti Sidona,

hautaweza kufanya sherehe tena;

hata ukikimbilia Kipuro,

kule nako hautapata pumziko!

13(Ni Wakaldea, wala si Waasuria, waliowaacha nyama wa pori waushambulie muji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia muji huo minara ya kuushambulia, wakabomoa nyumba zake na kuufanya mabomoko.)

14Mulie enyi mashua za Tarsisi,

maana kimbilio lenu limeharibiwa.

15Hapo muji wa Tiro utasahauliwa kwa muda wa miaka makumi saba, muda wa maisha ya mufalme. Kisha miaka hiyo makumi saba, muji wa Tiro utapatwa na kile watu wanachoimba juu ya kahaba:

16Kamata kinubi chako

uzungukezunguke ndani ya muji,

ewe kahaba uliyesahauliwa!

Imba nyimbo tamutamu.

Imba nyimbo nyinginyingi,

kusudi upate kukumbukwa tena.

17Kisha miaka hiyo makumi saba, Yawe atauazibu muji wa Tiro, nao utarudia kufanya uzinzi kwa kujiuzisha kwa mataifa yote ya dunia.

18Feza utakayopata itatakaswa kwa ajili ya Yawe. Hawatalinda feza hiyo lakini wale wanaomwabudu Yawe wataitumia kwa kununua chakula kingi na nguo nzuri.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help