1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2Wewe mwanadamu! Umugeukie Gogi mufalme wa inchi ya Magogi ambaye ni mutawala mukubwa wa Meseki na Tubali.
3Toa unabii juu yake na kumwambia kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe, ewe Gogi, mutawala wa Meseki na Tubali.
4Mimi nitakugeuza na kukutia ndoana katika mataya yako, na kukutoa inje wewe pamoja na kundi lako lote la waaskari: farasi na waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa la watu wanaovaa nguo za vita, ngao kubwa na ndogo katika mikono pamoja na mapanga yao.
5Kati yao kuna waaskari kutoka Persia, Etiopia na Puti; wote wana ngao na kofia za chuma.
6Vilevile makundi ya waaskari kutoka Gomeri, Beti Torgama, upande wa kaskazini kabisa, na makundi yao yote pamoja na makundi kutoka katika mataifa mengine, yako pamoja nawe.
7Ujitayarishe, uikae wewe mwenyewe na kundi lako lote pamoja na wengine wote unaokuwa nao, uwalinde.
8Kisha siku nyingi utaitwa kuishambulia inchi ambayo watu wengi waliletwa kutoka mataifa mengi na sasa wanaishi bila vitisho vya vita. Utaishambulia milima ya Israeli ambayo hapo zamani ilikuwa jangwa na matongo kwa muda murefu, lakini sasa watu wote huko wanaishi kwa usalama.
9Utakwenda mbio kama zoruba na kuifunika inchi kama wingu, wewe mwenyewe na kundi lako lote la waaskari pamoja na mataifa mengi yanayokuwa pamoja nawe.
10Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile, utaanza kuwaza ndani ya moyo wako na kupanga mipango miovu na kusema:
11Nitakwenda kuishambulia inchi isiyokuwa na kuta, inchi ambako wanainchi wake wanaishi kwa amani. Wote wanakaa katika miji isiyokuwa na kuta; hawana vifungio wala milango.
12Utanyanganya na kuteka mali za watu wanaokaa katika miji ambayo ilikuwa jangwa. Watu hao wamekusanywa kutoka katika mataifa na sasa wana makundi ya nyama na mali; nao wanakaa kwenye kitofu cha dunia.
13Wakaaji wa Seba na Dedani pamoja na wachuuzi wa Tarsisi na wa vijiji vyake watakuuliza: Umekuja kunyanganya? Umekusanya kundi lako la waaskari kwa kushambulia na kutwaa mateka na kubeba feza na zahabu, makundi ya nyama na vitu, na kuondoka na vitu vingi?
14Kwa hiyo, ewe mwanadamu, toa unabii na kumwambia Gogi kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Siku ile, taifa langu la Waisraeli litaishi kwa usalama, wewe utafunga safari
15kutoka kwenye makao yako, huko mbali kabisa upande wa kaskazini, ukuje pamoja na watu wengi wakiwa wote wamepanda farasi: jeshi kubwa na lenye nguvu.
16Utawashambulia Waisraeli, kama vile wingu linalotanda juu ya inchi. Wakati huo nitakutuma uishambulie inchi yangu, kusudi mataifa yajue kwamba nimekutumia wewe Gogi kusudi nionyeshe utakatifu wangu mbele yao.
17Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe ndiwe niliyesema habari zako hapo zamani kwa njia ya watumishi wangu manabii wa Israeli, ambao walitabiri nyakati zile kwamba nitakuleta kusudi ushambulie watu wa Israeli.
Mungu atamwazibu Gogi18Siku ile Gogi atakapoishambulia inchi ya Israeli, nitawakisha kasirani yangu.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
19Mimi ninasema wazi kwa wivu na kasirani yangu kali kwamba siku hiyo kutakuwa tetemeko kubwa la inchi katika inchi ya Israeli.
20Samaki na ndege, nyama wa pori, viumbe vyote vinavyotambaa pamoja na watu wote katika dunia, watatetemeka kwa kuniona. Milima itaporomoshwa, mawe yataanguka na kuta zote zitaanguka chini.
21Nami nitasababisha kila namna ya kitisho juu ya Gogi.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Waaskari wake wataanza kushambuliana wenyewe kwa mapanga yao.
22Nitamwazibu Gogi kwa ugonjwa mukali na mauaji. Nitanyesha mvua nyingi na mvua ya mawe na moto na kiberiti juu yake, juu ya makundi yake, na mataifa yale mengi yanayokuwa pamoja naye.
23Ndivyo nitakavyofanya kusudi yote yaone ukubwa wangu na utakatifu wangu. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.