1Watu walipoona kwamba Musa amechelewa kurudi kutoka juu ya mulima, wakakusanyika mbele ya Haruni na kumwambia: Basi! Ututengenezee miungu itakayotuongoza, maana hatujui jambo lililomupata yule Musa aliyetutoa katika inchi ya Misri.
2Haruni akawajibu: Mutwae pete za zahabu za masikio ya wake zenu, wana wenu na wabinti zenu, muniletee.
3Basi, watu wote wakatoa pete zote za zahabu za masikio yao, wakamuletea Haruni.
4Naye akazitwaa akaziyeyusha, akatengeneza sanamu ya mwana-ngombe.
Watu wakapaaza sauti wakasema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri.
5Kisha Haruni akamujengea yule mwana-ngombe mazabahu, halafu akatangaza: Kesho kutakuwa sikukuu kwa ajili ya Yawe.
6Kesho yake watu wakaamuka mapema wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Watu wakaikaa chini kwa kula na kunywa, kisha wakasimama na kucheza.
7Yawe akamwambia Musa: Teremuka chini kwa maana watu wako uliowaleta kutoka inchi ya Misri wamejipotosha wenyewe.
8Wameacha mara moja njia niliyowaamuru, wakajifanyia sanamu ya mwana-ngombe, nao wamemwabudu na kumutolea sadaka wakisema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri!
9Ninawafahamu watu hawa. Wao wana vichwa vigumu.
10Sasa, usijaribu kunizuia. Uniache niwaangamize kwa kasirani kali. Kisha kutokana nawe nitaunda taifa kubwa.
11Lakini Musa akamusihi Yawe, Mungu wake, akisema: Ee Yawe, kwa nini hasira yako inawaka vikali juu ya watu wako uliowatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo mukubwa na mukono wenye nguvu?
33Lakini Yawe akamwambia Musa: Nitamufuta katika kitabu changu mutu yeyote aliyenitendea zambi.
34Lakini sasa kwenda uwaongoze watu mpaka pahali nilipokuambia. Malaika wangu atakutangulia. Hata hivyo, siku nitakapowafikia, nitawaazibu kwa sababu ya zambi yao.
35Yawe akawaletea watu ugonjwa mukali, kwa kuwa walimwomba Haruni awafanyie yule mwana-ngombe wa zahabu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.