1Yosefu akamukumbatia baba yake akilia na kumubusu.
2Kisha, akawaagiza waganga wake wamupakae baba yake Israeli, dawa kusudi asioze, nao wakafanya hivyo.
3Kama kawaida, siku makumi ine zilihitajika kwa kazi hiyo. Wamisri nao wakaomboleza kifo cha Yakobo kwa muda wa siku makumi saba.
4Nyuma ya kilio kumalizika, Yosefu akawaambia watu wa jamaa ya mufalme wa Misri: “Ikiwa nimepata kukubaliwa mbele yenu, tafazali muzungumuze na mufalme kwa ajili yangu kwamba baba yangu aliniapisha, akisema:
5‘Mimi niko karibu kufa. Inakupasa kunizika katika kaburi nililojichongea katika inchi ya Kanana.’ Kwa hiyo ninamwomba aniruhusu niende kumuzika baba yangu, kisha nitarudi.”
6Mufalme akajibu: “Kwenda umuzike baba yako kama vile alivyokuapisha.”
7Basi, Yosefu akaondoka kwenda kumuzika baba yake akisindikizwa na watumishi wengi wa mufalme wa Misri, wazee wa nyumba ya mufalme, pamoja na wazee wa inchi nzima ya Misri.
8Vilevile, Yosefu alisindikizwa na jamaa yake yote, wandugu zake na jamaa yote ya baba yake Yakobo. Katika eneo la Goseni kulibaki watoto wao tu pamoja na kondoo, mbuzi na ngombe wao.
9Vilevile alisindikizwa na wapanda-farasi na magari, lilikuwa kundi kubwa sana.
10Walipofika katika uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, ngambo ya muto Yordani, waliomboleza kwa huzuni kubwa, naye Yosefu akamufanyia baba yake marehemu kilio cha siku saba.
11Wakanana wenyeji wa inchi hiyo, walipoona maombolezo yaliyofanyika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, wakasema: “Maombolezo haya ya Wamisri, kweli ni makubwa!” Kwa hiyo, pahali pale pakaitwa Abeli-Misri, napo pako ngambo ya muto Yordani.
12Wana wa Yakobo walimufanyia baba yao kama vile alivyowaagiza:
13wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.
14Nyuma ya kumuzika baba yake, Yosefu akarudi Misri pamoja na wandugu zake na watu wote waliokuwa wakimusindikiza kwenda kumuzika baba yake.
Yosefu anawaondolea wandugu zake shaka15Nyuma ya kifo cha baba yao, wandugu za Yosefu walisemezana: “Labda Yosefu atatuchukia na kutulipiza mabaya yote tuliyomutendea.”
16Kwa hiyo wakamupelekea Yosefu ujumbe, wakisema: “Baba yako, mbele hajakufa, aliagiza hivi:
17‘Mumwambie Yosefu kwa ajili yangu: Tafazali uwasamehe wandugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafazali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, akalia.
18Kisha wandugu zake wakamufikia, wakainama mpaka chini mbele yake, wakasema: “Sisi ni watumishi wako.”
19Lakini Yosefu akawaambia: “Musiogope, mimi ni pahali pa Mungu?
20Ninyi mulitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema kusudi watu wengi wapate kuwa wazima kama vile munavyoona leo.
21Basi, musiogope. Mimi nitawapa chakula pamoja na watoto wenu.” Basi akawafariji na kusema nao vizuri.
Kifo cha Yosefu22Yosefu akaendelea kukaa katika inchi ya Misri pamoja na jamaa yote ya baba yake. Aliishi kwa muda wa miaka mia moja na kumi.
23Yosefu alijaliwa kuwaona watoto na wajukuu wa mwana wake Efuraimu na vilevile kuwapokea kama wana wake watoto wa Makiri mwana wa Manase.
24Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”
25Kisha Yosefu akawaapiza wana wa Israeli, akisema: “Mungu atakapowafikia kwa kuwasaidia, muhakikishe kwamba mutapeleka mifupa yangu kutoka huku.”
26Basi, Yosefu akakufa kule Misri, akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi. Nao wakapakaa mwili wake dawa kusudi usioze, wakauweka katika sanduku kule Misri.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.