Mezali 6 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maonyo mane

1Mwana wangu, kama umejitolea kubeba deni ya mwenzako,

ikiwa umetoa ahadi yako kwa ajili ya mutu yule,

2ikiwa umejifunga kwa maneno yako mwenyewe,

utajinasa kwa ahadi uliyofanya;

3ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzako,

lakini mwana wangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi:

umwendee mutu yule mara moja, umusihi akupe uhuru wako.

4Usiache macho yako yapate usingizi,

wala kope za macho yako zisinzie.

5Ujiokoe kwa kujitoa katika mutego ule,

ujiponyeshe kama vile paa au ndege anayemutoroka mwindaji.

6Ewe muvivu! Kwenda kuchunguza siafu,

fikiri juu ya namna yake ya kuishi upate hekima.

7Siafu hana kiongozi, mukubwa, wala mutawala;

8lakini anajiwekea chakula wakati wa kipwa,

anajikusanyia akiba wakati wa mavuno.

9Ewe muvivu, utalala pale mpaka wakati gani?

Utaamuka wakati gani katika usingizi wako?

10Unasema: “Acha nilale kidogo tu,

acha nisinzie kidogo!

Uniache nikunje mikono nipumzike kidogo!”

11Wakati ule umasikini utakushambulia kama munyanganyi,

ukosefu utakufuata kama mwizi mwenye silaha.

12Mutu mwovu, mutu asiyefaa kitu,

anatangatanga akisema maneno mapotovu.

13Anakonyeza jicho kwa kuwakosesha wengine,

anaparuza kwa miguu

na kufanyia watu kitambulisho kwa vidole.

14Akiwa amejaa mabaya ndani ya moyo, anatunga maovu.

Anaamusha ugomvi kila pahali.

15Kutokana na hayo hasara itamupata kwa rafla;

kwa rafla atapondekana vibaya wala hatapata kupona.

16Kuna vitu sita Yawe anavyochukia,

hata saba ambavyo ni chukizo kwake:

17Macho ya kiburi,

ulimi mudanganyifu,

mikono inayoua wasiokuwa na kosa,

18moyo unaopanga mipango miovu,

miguu inayokuwa mbio kutenda maovu,

19mushuhuda wa uongo anayesema uongo,

na mutu anayechochea fitina kati ya wandugu.

Maonyo juu ya uasherati

20Mwana wangu, shika amri za baba yako,

wala usisahau mashauri ya mama yako;

21uyaweke siku zote ndani ya moyo,

uyafunge katika shingo lako.

22Yatakuongoza katika njia yako,

yatakulinda wakati unapolala,

yatakushauria unapoamuka.

23Maana amri hizi ni taa,

na shauri hilo ni mwangaza.

Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.

24Yatakulinda mbali na mwanamuke mubaya,

yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamuke mugeni.

25Usimutamani mwanamuke yule kwa uzuri wake,

wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.

26Mutu anapoteza kipande cha mukate kwa kahaba,

lakini mwanamuke muzinzi atapoteza uzima wako wote.

27Mutu anaweza kuweka moto kwenye kifua chake

na nguo zake zikose kuungua?

28Mutu anaweza kukanyaga makaa ya moto

na miguu yake ikose kuungua?

29Ndivyo mwanaume anayelala na muke wa mwenzake anavyokuwa;

yeyote anayemugusa mwanamuke yule hataacha kuazibiwa.

30Watu hawamuzarau sana mutu akiiba kwa sababu ya njaa,

31lakini akipatikana anapaswa kulipa mara saba,

tena atatoa mali yote anayokuwa nayo.

32Anayezini hana akili kabisa;

anajiangamiza yeye mwenyewe.

33Atapata vidonda na mazarau;

haya atakayopata haitatoka juu yake.

34Maana wivu wa mume unamufanya kuwa mukali kabisa;

wakati atakapolipiza kisasi hana kitu cha kuhurumia.

35Hatakubali malipo yoyote;

wala kutulizwa na zawadi zako nyingi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help