1-14Hayo ndiyo majina ya viongozi wa ukoo za watu waliorudi pamoja nami Ezra kutoka Babeli, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta:
Gersomi, wa ukoo wa Finehasi;
Danieli, wa ukoo wa Itamari;
Hatusi, wa ukoo wa Daudi;
mwana mumoja wa ukoo wa Sekania;
Zakaria, wa ukoo wa Parosi, pamoja na wanaume mia moja na makumi tano wa ukoo wake, walioandikishwa pamoja;
Eliyoenayi mwana wa Zerahia, wa ukoo wa Pahati-Moabu, pamoja na wanaume mia mbili;
Sekania mwana wa Yahasieli, wa ukoo wa Zatu, pamoja na wanaume mia tatu;
Ebedi mwana wa Yonatani, wa ukoo wa Adini, pamoja na wanaume makumi tano;
Yesaya mwana wa Atalia, wa ukoo wa Elamu, pamoja na wanaume makumi saba;
Zebadia mwana wa Mikaeli, wa ukoo wa Sefatia, pamoja na wanaume makumi nane;
Obadia mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Yoabu, pamoja na wanaume mia mbili kumi na wanane;
Selemoti mwana wa Yosifia, wa ukoo wa Bani, pamoja na wanaume mia moja na makumi sita;
Zakaria mwana wa Bebayi, wa ukoo wa Bebayi, pamoja na wanaume makumi mbili na wanane;
Yohanani mwana wa Hakatani, wa ukoo wa Azgadi, pamoja na watu mia moja na kumi;
Elifeleti, Yueli na Semaya, wa ukoo wa Adonikamu, pamoja na wanaume makumi sita, (hawa walirudi kisha);
Utayi na Zakuri, wa ukoo wa Bigwayi pamoja na wanaume makumi sita.
Ezra anatafuta Walawi kwa ajili ya hekalu15Nikawakusanya pamoja watu wote pembeni ya muto unaoelekea muji wa Ahava. Kule, tukapiga kambi kwa muda wa siku tatu. Nikaangalia kati ya watu wote pamoja na makuhani, lakini sikupata Walawi kati yao.
16Nikaita viongozi tisa wakuje kwangu: Eliezeri, Arieli, Semaya, Elnatani, Yaribu, Elnatani, Natani, Zekaria na Mesulamu, pamoja na waalimu wawili, Yoyaribu na Elnatani.
17Nikawatuma kwa Ido, kiongozi wa jamii ya watu kule Kasifia, nikimwomba yeye pamoja na wenzake watumishi wa nyumba ya Mungu, watuletee watu watakaotumika katika nyumba ya Mungu.
18Kwa neema ya Mungu, wakatuletea Serebia, mutu mwenye akili na Mulawi wa ukoo wa Mali, pamoja na wana wake na wandugu zake kumi na wanane.
19Wakatuletea vilevile Hasabia na Yesaya, wote wa ukoo wa Merari, pamoja na wandugu zao makumi mbili.
20Zaidi ya hao, kulikuwa watumishi wa hekalu mia mbili makumi mbili ambao babu zao walikuwa wamechaguliwa na mufalme Daudi na wakubwa wake kwa kuwasaidia Walawi. Majina ya watu wote hawa yameandikwa.
Watu wanaomba na kufunga21Kisha, nikatoa maagizo kuwa sisi wote tufike karibu na muto Ahara kusudi tufunge kula chakula na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wetu na kumwomba atulinde na kutuongoza katika safari yetu pamoja na watoto wetu.
22Ingekuwa haya kubwa kwangu kumwomba mufalme kundi la waaskari na waaskari wapanda-farasi wa kutulinda na waadui katika njia maana nilikuwa nimekwisha kumwambia kwamba Mungu wetu anawabariki wote wanaomutafuta, lakini anawachukia na kuwaazibu wote wanaomwacha.
23Kwa hiyo tukafunga na kumwomba Mungu atulinde, naye akayasikia maombi yetu.
Zawadi kwa ajili ya hekalu24Halafu kati ya makuhani waliokuwa viongozi nikachagua kumi na wawili: Serebia, Hasabia pamoja na wenzao kumi.
25Hawa nikawapimia kwa mizani feza, zahabu na vyombo ambavyo mufalme, washauri wake, wakubwa wake pamoja na watu wa Israeli walivyokuwa wamevitoa kwa ajili ya sadaka ya nyumba ya Mungu wetu.
26Hivi ndivyo vitu nilivyowapimia: feza toni makumi mbili na mbili, vyombo mia moja vya feza, uzito wake kilo makumi saba, zahabu kilo elfu tatu na mia ine,
27mabakuli makumi mbili ya zahabu, uzito wake kilo nane, vyombo viwili vya shaba nzuri iliyongaa yenye bei kama ya zahabu.
28Kisha nikawaambia: “Ninyi mumetakaswa mbele ya Yawe. Vilevile na vyombo vimetakaswa na feza na zahabu ni matoleo ya mapenzi kwa Yawe, Mungu wa babu zenu.
29Tafazali muvilinde na muvitunze mpaka mutakapovipima mbele ya makuhani wakubwa, Walawi na viongozi wa ukoo za Israeli, kule Yerusalema katika vyumba vya nyumba ya Yawe.”
30Basi, makuhani na Walawi wakatwaa feza, zahabu na vyombo vyote walivyopimiwa, kwa kuvipeleka katika Yerusalema ndani ya nyumba ya Mungu wetu.
31Katika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza, tukasafiri kutokea kwenye muto Ahava, kwenda Yerusalema. Mungu wetu alikuwa pamoja nasi, akatulinda na waadui na washambulizi katika njia.
32Tulipofika Yerusalema, tukapumzika kwa muda wa siku tatu.
33Katika siku ya ine, tukiwa ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tukapima ile feza, zahabu na vile vyombo, kisha tukavipatia kuhani Meremoti mwana wa Uria. Meremoti alikuwa pamoja na Eleazari mwana wa Finehasi, na Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yesua, na Noadia mwana wa Binui.
34Kila kitu kilihesabiwa na kupimwa na wakati huo uzito wa kila kitu uliandikwa.
35Kisha, watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakamutolea Mungu wa Israeli sadaka zao za kuteketezwa kwa moto. Wakatoa ngombe dume kumi na wawili kwa ajili ya Israeli yote, kondoo dume makumi kenda na sita na wana-kondoo makumi saba na saba; vilevile walitoa mbuzi kumi na wawili kama sadaka ya kusamehewa zambi. Nyama wote hawa walitolewa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe.
36Vilevile wakawapa wasimamizi wa mufalme na watawala wa mukoa wa majimbo ya upande wa magaribi wa muto Furati maagizo waliyopewa na mufalme, nao wakatoa musaada kwa watu na kwa ajili ya nyumba ya Mungu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.