Yeremia 42 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wanainchi wanamusihi Yeremia awaombee

1Kisha wakubwa wote wa waaskari, Yohanani mwana wa Karea, na Azaria mwana wa Hosaya pamoja na watu wote, wadogo kama vile wakubwa,

2wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.

3Yawe, Mungu wako, atuonyeshe njia anayotaka tuifuate, na kile anachotaka tufanye.

4Yeremia akawajibu: Vema; nimesikia. Nitamwomba Yawe, Mungu wenu, kama mulivyonisihi; jibu lolote Yawe atakalonipa, nitawaambia; sitawaficha kitu chochote.

5Kisha, watu wakamwambia Yeremia: Yawe akuwe mushuhuda wa kweli na mwaminifu juu yetu ikiwa hatutafanya jinsi Yawe, Mungu wako atakavyokuagiza utuambie.

6Ikuwe ni jambo la kupendeza au hapana, sisi tutaitii sauti ya Yawe, Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake kusudi mambo yatuendekee vizuri tutakapomutii Yawe, Mungu wetu.

7Nyuma ya siku kumi, neno la Yawe lilimufikia Yeremia.

8Basi, Yeremia akamwita Yohana mwana wa Karea, na wakubwa wote wa waaskari pamoja na watu wote, wadogo kama vile wakubwa, akawaambia:

9Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninyi mulinituma kwake nipeleke maombi yenu, anasema hivi:

10Kama ninyi mutabaki katika inchi hii, basi, nitawasimamisha, wala sitawaharibu; nitawaotesha wala sitawaongoa; kwa maana nitabadilisha nia kwa sababu ya hasara niliyowatendea.

11Musimwogope mufalme wa Babeli munayemwogopa; musimwogope hata kidogo. Mimi niko pamoja nanyi kwa kuwaokoa na kuwaponyesha kutoka katika mikono yake.

12Nitawahurumia na kumufanya mufalme awahurumie na kuwaacha katika inchi yenu.

–Ni ujumbe wa Yawe.

13Lakini mukisema: Hatutaki kubaki katika inchi hii, na hivyo mukiacha kutii sauti ya Yawe, Mungu wenu,

14na kusema kwamba mutakwenda kukaa katika inchi ya Misri, ambako hamutaona vita wala kusikia sauti ya baragumu wala kukosa chakula,

15basi, musikilize jinsi Yawe anavyosema enyi mabaki ya Yuda. Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama mumekusudia kwenda katika inchi ya Misri na kukaa huko,

16basi, vita munavyoviogopa vitawakuta kulekule Misri, na njaa munayoogopa itawaandama vikali mpaka Misri, na mutakufia kulekule.

17Watu wote wenye nia ya kwenda kukaa Misri watakufa kwa njaa na ugonjwa mukali wala hakuna hata mumoja wao atakayebaki au kuponyoka kutokana na hasara nitakayowaletea.

18Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama vile hasira yangu na kasirani yangu ilivyowapata wakaaji wa Yerusalema, ndivyo kasirani yangu itakavyowapata ninyi, kama mutakwenda Misri. Mutakuwa kitu cha kutukaniwa, kitisho, laana na haya. Hamutaona tena nafasi hii.

19Yeremia akawaambia watu: Enyi Wayuda muliobaki, Yawe aliwaambia musiende Misri. Mujue wazi kwamba leo nimewaonya kwamba

20mumepotoka, mumeyahatarisha maisha yenu. Maana mulinituma kwa Yawe, Mungu wenu, mukiniambia: Utuombee kwa Yawe, Mungu wetu kwamba kitu chochote Yawe, Mungu wetu, atakachosema, utuambie, nasi tutatimiza.

21Leo mimi nimewaambia, lakini hamukutii neno lolote ambalo Yawe, Mungu wenu amenituma niwaambie.

22Basi, mujue hakika kwamba mutauawa kwa vita, kwa njaa na kwa ugonjwa mukali katika inchi ile munayotaka kwenda kukaa ndani yake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help