1Mwanadamu ana magumu katika dunia,
na siku zake ni kama siku za mutumishi wa mushahara!
2Yeye ni kama mutumwa anayetamani kivuli,
kama mutumishi anayengoja kwa hamu mushahara wake.
3Basi nimepangiwa miezi na miezi ya taabu,
urizi wangu ni kuteseka usiku kwa usiku.
4Ninapolala ninasema: “Nitaamuka wakati gani?”
Maana saa za usiku ni ndefu sana;
ninagaagaa katika kitanda mpaka mapambazuko!
5Mwili wangu umejaa vidudu na uchafu;
ngozi yangu imekauka na kutokwa na usaha wa jipu.
6Siku zangu zinapita mbio kuliko gurudumu la mushonaji,
nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
7Kumbuka, maisha yangu ni pumzi tu;
jicho langu halitaona jambo zuri lolote tena.
8Anayeniona sasa, hataniona tena,
mara tu ukiniangalia nitakuwa nimetoweka.
9Kama vile wingu linavyofifia na kutoweka,
ndivyo nao watu wanavyoshukia kuzimu bila kurudi.
10Anayeondoka harudi tena kwa jamaa yake,
na pale alipokuwa anaishi, wanamusahau mara moja.
11Kwa hiyo sitakizuia kinywa changu kusema.
Nitasema kwa kusongwa kwa roho yangu,
nitalalamika kwa uchungu wa nafsi yangu.
12Mimi ni bahari au nyama mukubwa wa bahari
hata upate kuniwekea mulinzi?
13Nikisema “Kitanda kitanipumzisha,
matandiko yangu yatanipunguzia malalamiko yangu”,
14wewe unakuja kunitia hofu kwa ndoto,
unanitisha kwa kuniletea maono,
15hata ninaona afazali kutundikwa,
ninaona heri kufa kuliko kupata mateso haya.
16Ninayachukia maisha yangu.
Sitaishi milele.
Muniache, maana siku zangu ni pumzi tu!
17Mwanadamu ni nini hata umujali?
Kwa nini unajishugulisha naye
18na kuja kumuchunguza kila asubui,
na kumupima kila wakati?
19Utaendelea kuniangalia mpaka wakati gani,
bila kuniacha hata nimeze mate?
20Kama nikitenda zambi,
inakuuzi nini, ewe muchungaji wa wanadamu?
Mbona umeniweka kuwa shabaha ya mapigo yako?
Kwa nini nimekuwa muzigo kwako?
21Mbona haunisamehe kosa langu
na kuniondolea uovu wangu?
Hivi kisha muda kidogo nitalazwa chini katika mavumbi.
Utanitafuta, lakini sitakuwa tena!
Masemi ya BildadiWho We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.