1“Mujiangalie musifanye matendo mema mbele ya watu kusudi mujionyeshe kwao. Kwa maana mukifanya hivi hamutapata faida kutoka kwa Baba yenu anayekuwa mbinguni.
2“Basi wakati unapomusaidia masikini, usipige baragumu, kama vile wanafiki wanavyofanya katika nyumba za kuabudia na katika barabara kusudi wasifiwe na watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.
3Lakini wewe, unapomusaidia masikini, ufanye tendo lile kwa uficho hata rafiki yako wa kweli asijue.
4Hivi tendo lile halitatoka inje, naye Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.
Mafundisho juu ya maombi(Lk 11.2-4)5“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.
6Lakini wewe, unapoomba, ingia ndani ya chumba chako, funga mulango na uombe kwa Baba yako asiyeonekana. Na Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.
7“Tena munapoomba, musitumie maneno mengi yasiokuwa na maana kama vile wapagani wanavyofanya, kwa sababu wanawaza kama Mungu atawasikia kama wakisema maneno mengi.
8Basi musifanye kama wao, musifanane nao kwa maana Baba yenu anajua vitu munavyohitaji mbele hamujamwomba.
9Basi muangalie namna munavyopaswa kusema munapoomba:
‘Baba yetu unayekuwa mbinguni,
Jina lako litukuzwe;
10Ufalme wako ukuje;
mapenzi yako yafanyike katika dunia kama inavyokuwa mbinguni.
11Utupe chakula chetu cha kila siku.
12Utusamehe makosa yetu,
kama sisi tunavyowasamehe wanaotukosea,
13Usituache kuanguka katika majaribu,
lakini utuokoe na yule Mwovu.
[Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu
ni vyako hata milele. Amina.]’
14“Hivi, mukiwasamehe watu wengine makosa wanayowatendea, Baba yenu anayekuwa mbinguni atawasamehe vilevile.
15Lakini kama musipowasamehe wengine wanaowakosea, Baba yenu hatawasamehe makosa yenu vilevile.
Mafundisho juu ya kufunga kula chakula16“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.
17Lakini wewe unapofunga kula chakula, unawe uso wako na kuchanua nywele zako,
18kusudi usijionyeshe kwa watu kwamba unafunga. Jambo hilo litajulikana tu kwa Baba yako anayekuwa kwa siri. Naye Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.
Akiba ya dunia na ya mbinguni(Lk 12.33-34)19“Musijiwekee akiba katika dunia hii, pahali nondo na kutu vinapoharibu, nao wizi wanapotoboa nyumba na kuiba.
20Lakini mujiwekee akiba katika mbingu, pahali nondo wala kutu visipoweza kuharibu, nao wizi wasipoweza kutoboa na kuiba.
21Kwa maana pahali akiba yako inapokuwa, ni pale roho yako inapokuwa vilevile.
Mwangaza wa mwili(Lk 11.34-36)22“Macho ni taa ya mwili. Kama macho yako yakiwa mazima, mwili wako wote utabaki katika mwangaza.
23Lakini kama macho yako yanaharibika, mwili wako wote utabaki katika giza. Basi ikiwa mwangaza unaokuwa ndani yako umegeuka kuwa giza, giza hilo ni nzito sana!
Mungu na mali(Lk 16.13)24“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.
Kutumainia Mungu(Lk 12.22-31)25“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.
26Muangalie ndege wanaoruka katika anga: wao hawapandi mbegu wala hawavuni, wala hawaweki mavuno ndani ya gala, lakini Baba yenu anayekuwa mbinguni anawakulisha! Basi ninyi si wa lazima zaidi kuliko ndege wale?
27Nani kati yenu, kwa ajili ya kujisumbua kwake, anaweza kujiongezea hata siku moja kupita muda wa maisha yake?
28“Kwa sababu gani munajisumbua kwa ajili ya nguo? Muangalie maua jinsi yanavyoota. Hayatumiki wala kujisukia nguo.
29Lakini ninawaambia kwamba hata mufalme Solomono katika utukufu wote aliokuwa nao hakuvaa nguo inayoweza kulinganishwa na uzuri wa moja la maua yale.
30Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana leo na kesho yanatoweka na kutupwa katika moto, hatawavalisha ninyi vizuri zaidi, ninyi wenye imani ndogo?
31“Basi musijisumbue kwa ajili ya chakula, kwa ajili ya kinywaji au kwa ajili ya nguo.
32Ni wapagani ndio wanaoshugulika kwa kutafuta vitu vile vyote. Baba yenu anayekuwa mbinguni anajua kama munahitaji vitu vile vyote.
33Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.
34Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.