1Kulipokwisha kupita miaka kumi na mine, nikarudia Yerusalema pamoja na Barnaba; nami nilikuwa pamoja na Tito vilevile.
2Nilienda kule kufuatana na agizo nililopata katika maono. Halafu nikakusanyika na waongozi kwa upekee. Nikawaelezea Habari Njema ninayohubiri kati ya mataifa mbalimbali kusudi kazi yangu ya mbele au ya sasa isipotee bure.
3Na Tito aliyesafiri pamoja nami hakulazimishwa kutahiriwa ingawa alikuwa Mugriki,
4ijapokuwa wandugu wamoja wa uongo waliojiunga nasi kwa kisirisiri walitaka kumutahiri. Watu hao walijiingiza katika kikundi kusudi wapate kupeleleza jinsi tunavyoishi katika uhuru kutokana na kuungana kwetu na Yesu Kristo. Walitaka kututia katika maisha ya kitumwa.
5Lakini hatukukubali kuwatii watu wale hata kidogo, kusudi ukweli wa Habari Njema uendelee kuchungwa kati yenu siku zote.
6Lakini kuelekea wale waliohesabiwa kuwa waongozi, hainifalii kitu kujua cheo gani walichokuwa nacho, kwa maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya inje. Watu wale hawakunifundisha kitu kipya.
7Lakini walitambua kuwa Mungu amenipatia kazi ya kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine sawa alivyomupatia Petro kazi ya kuihubiri kwa Wayuda.
8Kwa maana yule aliyemuwezesha Petro kuwa mutume kwa Wayuda, ndiye aliyeniwezesha vilevile kuwa mutume kwa watu wa mataifa mengine.
9Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.
10Lakini kitu kimoja walichotuomba ni kukumbuka wamasikini wa makanisa yao, nami nimefanya vile kwa bidii.
Paulo anaonya Petro katika Antiokia11Petro alipofika Antiokia, nilibishana naye waziwazi, kwa sababu alikuwa akidanganyika.
12Kwa maana mbele ya kufika kwa watu wamoja waliotumwa na Yakobo kule, yeye alizoea kula pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini watu wale walipofika, akajitenga na kuacha kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa sababu ya kuogopa wale wanaolazimisha kutahiriwa.
13Na waamini wengine Wayuda wakaanza kutenda kwa unafiki sawa Petro, na hata Barnaba akajiunga nao katika huo unafiki wao.
14Wakati nilipoona kwamba walikuwa wakitembea kinyume cha ukweli wa Habari Njema, nikamwambia Petro hivi mbele ya watu wote: “Ikiwa wewe unayekuwa Muyuda unafuata desturi za watu wa mataifa mengine, namna gani unaweza kuwalazimisha watu wa mataifa mengine wafuate desturi za Wayuda?”
Watu wa mataifa mengine wanaokolewa kwa njia ya kuamini Yesu15Hakika sisi Wayuda wa kizalikio hatuko watu wa mataifa mengine, hao wenye zambi.
16Lakini, tunajua kwamba mutu hahesabiwi haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria, lakini kwa njia ya kuamini Yesu Kristo. Sisi vilevile tumeamini Yesu Kristo kusudi tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika yeye, wala si kwa njia ya kushika Sheria. Ni vile kwa maana hakuna mutu atakayehesabiwa haki kwa njia ya kushika Sheria.
17Sasa tunapotafuta kuhesabiwa haki katika kuungana na Kristo, inaonekana kwamba sisi nasi ni wenye zambi sawa watu wa mataifa mengine. Jambo hili linaonyesha ya kama Kristo anatumika kwa ajili ya kuendelesha zambi? Hapana hata kidogo!
18Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha kubomoa, basi ninahakikisha kwamba mimi nimevunja Sheria.
19Maana kufuatana na Sheria hiyo, mimi nimekuwa kama mufu, na kifo kile kimesababishwa na Sheria. Imetokea vile kusudi nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimekufa pamoja na Kristo juu ya musalaba.
20Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.
21Mimi sitaki kukataa neema ya Mungu kwa maana ikiwa wanaweza kuhesabiwa haki mbele ya Mungu, kwa njia ya kushika Sheria, basi Kristo alikufa bure.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.