1 Wakorinto 13 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Hata nikiwa na uwezo wa kusema luga za watu na za wamalaika, lakini kama sina upendo, masemi yangu ni bure kama vile kelele la kengele au matoazi.

2Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure.

3Ninaweza vilevile kugawanya mali yangu yote kwa kulisha wamasikini na hata kutoa mwili wangu uunguzwe, lakini kama sina upendo, hakuna faida ninayopata.

4Upendo unavumilia, ni wenye wema; upendo hauna wivu, upendo haujivuni, na hauna kiburi.

5Upendo haukosi kuwa na adabu, hautafuti faida yake mwenyewe, haukasiriki upesi, nao hauhesabii mutu ubaya.

6Upendo haufurahii ubaya, lakini unafurahia ukweli.

7Upendo hauchoki na mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote na kuvumilia mambo yote.

8Upendo haukomi hata kidogo. Lakini kutabiri kunatoweka, zawadi ya kusema kwa luga za ajabu inatoweka, na maarifa yanapita.

9Kwa maana tunafahamu tu mambo machache na kutabiri tu mambo machache.

10Lakini wakati mambo matimilifu yatakapokuja, yale yasiokuwa matimilifu yatatoweka.

11Wakati nilipokuwa mutoto, nilisema kama mutoto, niliwaza kama mutoto, nilifikiri kama mutoto. Lakini nilipokuwa mutu muzima niliacha mambo ya kitoto.

12Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.

13Basi sasa, hivi vitu vitatu vinadumu: imani, tumaini na upendo; lakini kinachokuwa kikubwa kuliko hivi vingine ni upendo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help