Zaburi 124 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu ni mulinzi wetu

1Wimbo wa safari za kidini.

Ninyi wote munaokuwa katika Israeli museme:

“Kama Yawe asingalikuwa upande wetu”.

2“Kama Yawe asingalikuwa upande wetu,

wakati ule tuliposhambuliwa na waadui,

3hakika tungalimezwa tukikuwa wazima,

wakati hasira yao ilipowaka juu yetu.

4Tungalichukuliwa na maji mengi,

tungalifunikwa na muto.

5Tungalizamishwa na maporomoko ya maji!”

6Yawe atukuzwe!

Hakutuachilia katika meno yao.

7Tumeponyoka kama ndege katika mutego;

mutego umefyatuka, nasi tukaponyoka.

8Musaada wetu unatoka kwa Yawe,

aliyeumba mbingu na dunia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help