1Hekima amejenga nyumba yake,
nyumba yenye nguzo saba.
2Amechinja nyama wa karamu,
divai yake ameitayarisha,
ametandika meza yake.
3Amewatuma wajakazi wake katika muji
waite watu kutoka kwenye vilele vya milima:
4“Yeyote anayekuwa mujinga akuje hapa!”
Na yeyote anayekuwa mupumbafu unamwambia:
5“Kuja ukule chakula,
na ukunywe divai niliyotengeneza.
6Achana na ujinga upate kuishi;
fuata njia ya akili.”
7Anayemwonya mwenye kiburi anapata mazarau,
anayekaripia mwovu anajiletea matusi.
8Usimwonye mwenye kiburi maana atakuchukia;
umwonye mwenye hekima naye atakupenda.
9Umufundishe mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima;
umufundishe mutu wa haki naye atazidi kuwa na elimu.
10Kumwogopa Yawe ni musingi wa hekima;
na kumujua yule Mutakatifu ni kupata akili.
11Kwa musaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa;
utaongezewa miaka mingi katika maisha yako.
12Kama una hekima, itakufaa wewe mwenyewe;
kama ukiizarau, wewe mwenyewe utapata hasara.
13Mwanamuke mupumbafu ana kelele,
hajui kitu wala hana haya.
14Anaikaa kitako kwenye mulango wa nyumba yake,
anaweka kiti chake pahali pa juu katika muji,
15na kuwaita watu wanaopita katika njia,
watu wanaokwenda kwenye shuguli zao:
16“Yeyote anayekuwa mujinga akuje hapa!”
Na yeyote anayekuwa mupumbafu anamwambia:
17“Maji yaliyoibwa ni matamu sana;
mukate unaokuliwa kwa siri ni muzuri sana.”
18Lakini mujinga hajui kwamba mule muna wafu,
wageni wa mwanamuke yule wako chini katika kuzimu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.