Walawi 27 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Sheria juu ya matoleo

1Yawe akamwambia Musa:

2Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu akifanya kiapo cha kumutolea Yawe mwanadamu, mutu huyu anaweza kuondoa kiapo chake kwa kulipa kipimo cha feza kinachokadiriwa kama hivi:

3Mwanaume wa miaka makumi mbili mpaka miaka makumi sita atakombolewa kwa feza shekeli makumi tano kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu.

4Kama ni mwanamuke, atakombolewa kwa feza shekeli makumi tatu.

5Kama mutu huyu ni wa miaka kati ya mitano na makumi mbili atakombolewa kwa feza shekeli makumi mbili kama ni kijana na shekeli kumi za feza kama ni binti.

6Ikiwa ni mutoto wa umri wa kati ya mwezi mumoja na miaka mitano atakombolewa kwa shekeli tano za feza kama ni kijana na shekeli tatu za feza kama ni binti.

7Ikiwa mutu huyu umri wake ni zaidi ya miaka makumi sita, bei yake itakuwa ni shekeli kumi na tano za feza, kama ni mwanaume na shekeli kumi za feza kama ni mwanamuke.

8Lakini ikiwa mutu huyu ni masikini na hawezi kulipa malipo yake, basi, mutu yule atapelekwa kwa kuhani. Kuhani atapima bei yake kulingana na uwezo wa huyo aliyefanya kiapo.

9Ikiwa kiapo chenyewe kinaelekea nyama wa namna ambayo watu wanamutolea Yawe sadaka, basi nyama huyo anakuwa kitu kitakatifu.

10Hairuhusiwi kumubadilisha nyama huyo na mwingine yeyote, muzuri kwa mubaya au mubaya kwa muzuri. Kama akimubadilisha na nyama mwingine, wote wawili watakuwa watakatifu.

11Kama kiapo hicho kinaelekea nyama muchafu wa aina ambayo hairuhusiwi kumutolea Yawe, basi, mutu aliyemutoa, atamuleta kwa kuhani,

12naye kuhani ataamua bei yake kulingana na uzuri au ubaya wake. Jinsi kuhani atakavyoamua, ndivyo itakavyokuwa.

13Lakini ikiwa mwenyeji anataka kumukomboa, basi, ataongeza asili mia makumi mbili ya bei ya nyama huyo.

14Mutu akitakasa nyumba yake kuwa takatifu kwa Yawe, kuhani ataamua bei yake kulingana na uzuri au ubaya wake. Jinsi atakavyoamua, ndivyo itakavyokuwa.

15Kama huyo mutu aliyeitakasa akitaka kuikomboa hiyo nyumba, basi, ataongeza asili mia makumi mbili ya bei yake, nayo itakuwa mali yake.

16Mutu akitakasa shamba lake, ambalo ni urizi wake, kwa ajili ya Yawe, basi, bei yake itapimwa kulingana na mbegu zinazotumiwa kwa kupanda shamba hilo. Kwa kila kilo makumi mbili za shayiri bei yake itakuwa shekeli makumi tano za feza.

17Kama akitakasa shamba lake katika mwaka wa kukumbuka miaka makumi tano, bei yake ilingane na vipimo vyenu.

18Lakini kama akilitakasa kisha mwaka huo, basi, kuhani ataamua bei yake kulingana na miaka inayobaki kufikia mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano na bei yake ipunguzwe.

19Kama mwenyeji akitaka kulikomboa, basi, aongeze asili mia makumi mbili ya bei ya shamba hilo, na kisha litakuwa mali yake.

20Lakini kama hataki kulikomboa au amemwuzishia mutu mwingine, basi, shamba hilo lisikombolewe tena.

21Katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano shamba hilo litaachiliwa na kuwa la Yawe milele. Kuhani ndiye atakayelirizi.

22Kama mutu akitakasa shamba alilonunua, ni kusema sio lake kwa urizi,

23kuhani ataamua bei ya shamba hilo kwa kulingana na miaka inayobaki kufikia mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano na mutu huyo atalipa bei yake kama ni kitu kitakatifu kwa Yawe.

24Lakini katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makuni tano, shamba hilo lirudishiwe yule mutu aliyeliuzisha.

25Kila bei itapimwa kwa kipimo cha uzito cha shekeli kulingana na kipimo cha Pahali Patakatifu: uzito wa gera makumi mbili ni sawa na uzito wa shekeli moja.

26Hairuhusiwi kumutakasa muzaliwa wa kwanza wa nyama. Kufuatana na sheria, huyo ni wa Yawe, akuwe ni ngombe au kondoo.

27Kama ni nyama muchafu, mwenyeji atamununua kwa kulingana na jinsi munavyomupima na ataongeza asili mia makumi mbili ya bei ya nyama huyo. Kama hakombolewi, basi atauzishwa kulingana na vipimo vyenu.

28Lakini kitu chochote kilichotakaswa kwa Yawe, kama ni mutu au nyama au kitu kilichopatikana kwa urizi, hakitauzishwa wala kukombolewa. Chochote kilichotakaswa kwa Yawe ni kitakatifu kabisa. Ang. Hes 18.14

29Mutu yeyote aliyetakaswa kwa Yawe asikombolewe. Sharti auawe.

30Zaka za mazao ikuwe ni ngano au matunda ya miti, yote ni mali ya Yawe. Yote ni takatifu kwa Yawe. Ang. Hes 18.21; Kumb 14.22-29

31Kama mutu akitaka kukomboa zaka yake, atalipa bei yake na kuongeza asili mia makumi mbili ya bei ya zaka hiyo.

32Kuelekea mifugo, kila nyama wa kumi ni mutakatifu kwa Yawe.

33Mutu yeyote hana ruhusa ya kuuliza kama nyama huyo ni muzuri au mubaya wala nyama huyo hatabadilishwa na mwingine. Kama akibadilishwa na mwingine, nyama wote wawili watakuwa watakatifu. Hawatakombolewa.

34Hizo ndizo amri ambazo Yawe alimwamuru Musa kusudi awaambie Waisraeli kwenye mulima Sinai.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help