1Hawa ndio wazao wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli. (Ingawa Rubeni alikuwa muzaliwa wa kwanza haki yake ya muzaliwa wa kwanza ilipewa kwa ndugu yake Yosefu kwa sababu Rubeni alilala na habara wa baba yake. Kwa hiyo, yeye hakutiwa katika hesabu ya ukoo kulingana na haki yake ya muzaliwa wa kwanza.
3Wana wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: Hanoki, Palu, Hesironi na Karmi.
4Wazao wa Yoeli toka kizazi mpaka kizazi kingine walikuwa: Semaya, Gogo, Simei,
5Mika, Raya, Bali,
6na Bera, ambaye mufalme Tigilati-Pileseri wa Asuria, alimukamata mateka ingawa alikuwa kiongozi wa watu wa kabila la Rubeni, akamupeleka katika uhamisho.
7Wakubwa wa ukoo hizi ndio walioandikwa katika kitabu cha vizazi vya kabila la Rubeni: Yeieli, Zekaria,
8Bela mwana wa Ahazi na mujukuu wa Sema, wa ukoo wa Yoeli, uliokuwa ukiishi Aroeri na katika eneo lote la upande wa kaskazini mpaka Nebo na Bali-Meoni.
9Vilevile, kwa maana makundi yao ya nyama iliongezeka kwa wingi sana, walisambaa upande wa mashariki mpaka kwenye viingilio vya jangwa lililoenea mpaka kwenye muto Furati.
10Katika siku za utawala wa mufalme Saulo, kabila la Rubeni wakapigana vita na Wahagari, wakawaua katika vita na kutwaa inchi yao yote upande wa mashariki wa Gileadi, wakaishi mule.
Wazao wa Gadi11Kabila la Gadi lilikuwa na mupaka na kabila la Rubeni upande wa kaskazini, katika inchi ya Basani iliyoenea upande wa mashariki mpaka Saleka.
12Pale kulikuwa ukoo za: Yoeli, uliokuwa ukoo mukubwa zaidi; Safamu, ndio wa pili; Yanai; na Sefati kule Basani.
13Ndugu zao kulingana na ukoo zao walikuwa saba: Mikaili, Mesulamu, Seba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
14Wote hawa walikuwa wana wa Abihaili, aliyekuwa mwana wa Huri. Huri alikuwa mwana wa Yaroa, Yaroa wa Gileadi, Gileadi wa Mikaili, Mikaili wa Yesisai, Yesisai wa Yado, na Yado wa Buzi.
15Ahi, aliyekuwa mwana wa Abudieli na mujukuu wa Guni, alikuwa mukubwa katika ukoo hizi.
16Waliishi katika sehemu ya Gileadi, katika Basani na miji yake na katika mashamba ya malisho yote ya Saroni, hata kwenye mipaka.
17Watu hao wote waliandikwa katika ukoo, katika siku za utawala wa Yotamu, mufalme wa Yuda, na Yeroboamu, mufalme wa Israeli.
Majeshi ya makabila ya upande wa mashariki18Makabila ya Rubeni, Gadi na Manase ya upande wa mashariki, yalikuwa na waaskari shujaa yapata elfu makumi ine na ine mia saba na makumi sita, wenye ngao na mapanga, wavuta pinde wafundi katika vita.
19Walipigana vita na makabila ya Wahagari, Yeturi, Nafisi na Nodabu.
20Waliweka tumaini lao kwa Mungu na wakamwomba awasaidie, naye akaitikia ombi lao na kuwatia katika mikono yao Wahagari pamoja na warafiki zao.
21Walinyanganya ngamia elfu makumi tano, kondoo elfu mia mbili na makumi tano, punda elfu mbili na kuwapeleka watu elfu mia moja kuwa wafungwa.
22Wakaua waadui wengi sana kwa sababu vita hiyo ilikuwa ni vita ya Mungu. Nao waliendelea kuishi katika inchi ile, mpaka wakati wa uhamisho.
Nusu ya wazao wa Manase23Nusu ya watu wa kabila la Manase waliishi katika inchi ya Basani. Hesabu yao iliongezeka kwa wingi sana, wakasambaa upande wa kaskazini mpaka Bali-Hermoni, Seniri na mulima Hermoni.
24Hawa ndio waliokuwa wakubwa wa ukoo za kabila lile: Eferi, Isi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yadieli. Wote walikuwa waaskari shujaa, watu wenye heshima sana na viongozi katika ukoo hizo.
Makabila ya upande wa mashariki yanapelekwa katika utumwa25Lakini watu wakamwasi Mungu wa babu zao, wakafanya uzinzi kwa kuabudu miungu ya wakaaji wa inchi zile ambazo Mungu aliangamiza mbele yao.
26Basi, Mungu wa Israeli akasukuma roho ya Puli, mufalme wa Asuria, (ambaye alijulikana vilevile kwa jina la Tiglati-Pileseri), akashambulia inchi yao na kuwapeleka watu wa kabila la Rubeni, la Gadi na nusu ya kabila la Manase kwa upande wa mashariki mpaka uhamisho kule Hala, Habori na Hara, pembeni ya muto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo. Wazao wa Lawi
27Lawi alikuwa na wana watatu: Gersoni, Kohati na Merari.
28Kohati alikuwa na wana wane: Amuramu, Izihari, Hebroni na Usieli.
29-40Amuramu alikuwa na wana wawili: Haruni na Musa, na binti mumoja jina lake Miriamu.
Haruni alikuwa na wana wane: Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.
Eleazari alizaa Finehasi,
Finehasi alizaa Abisua,
Abisua alizaa Buki,
Buki alizaa Usi,
Usi alizaa Zerahia,
Zerahia alizaa Merayoti,
Merayoti alizaa Amaria,
Amaria alizaa Ahitubu,
Ahitubu alizaa Zadoki,
Zadoki alizaa Ahimasi,
Ahimasi alizaa Azaria,
Azaria alizaa Yohana,
Yohana alizaa Azari aliyefanya kazi ya ukuhani katika hekalu mufalme Solomono alilojenga kule Yerusalema,
Azaria alizaa Amaria,
Amaria alizaa Ahitubu,
Ahitubu alizaa Zadoki,
Zadoki alizaa Mesulamu,
Mesulamu alizaa Hilkia,
Hilkia alizaa Azaria,
Azaria alizaa Seraya,
Seraya alizaa Yozadaki.
41Yozadaki alikwenda katika uhamisho wakati Yawe alipowapeleka katika uhamisho watu wa inchi ya Yuda na Yerusalema kwa kutumia mukono wa mufalme Nebukadneza.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.