1Zaburi ya Asafu. Wimbo.
2Ee Mungu, usikae kimya!
Usinyamaze, ee Mungu, wala usitulie!
3Angalia! Waadui zako wanafanya fujo;
wanaokuchukia wanainua vichwa kwa kiburi.
4Wanafanya mipango mibaya kwa kuwazuru watu wako;
wanashauriana juu ya hao unaowalinda.
5Wanasema: “Mukuje tuangamize taifa lao,
hata jina la Israeli lisikumbukwe tena.”
6Kweli, wanakubaliana kwa moyo moja,
wanafanya mapatano juu yako:
7Waedomu na Waisimaeli,
Wamoabu na Wahagari;
8Wagebali, Waamoni na Waamaleki,
Wafilistini na wakaaji wa Tiro.
9Hata Waasuria wameshirikiana nao,
wamewaunga mukono wazao wa Loti!
10Uwatendee ulivyowatendea Wamidiani,
ulivyowatendea Sisera na Mufalme Asikie
kwenye muto Kisoni,
11watu uliowaangamiza kule Endori,
wakakuwa takataka juu ya inchi.
12Uwatendee wakubwa na watawala wao
kama Kibombobombo na Mbwa wa Pori,
kama Sadaka na Kivuli,
13ambao walisema: “Tutajitwalia inchi ya Mungu.”
14Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi;
kama makapi yanayopeperushwa na upepo.
15Kama vile moto unavyoteketeza pori,
na ndimi za moto zinavyounguza milima,
16uwakimbize hao kwa zoruba yako,
na kuwatisha kwa upepo wako mukali!
17Ujaze nyuso zao haya,
wapate kukutafuta, ee Yawe.
18Wafezeheke na kuhangaika milele,
waangamie kwa haya kabisa.
19Wajue kwamba wewe peke yako,
ambaye jina lako ni Yawe,
ndiwe Mungu Mukubwa juu ya dunia yote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.