Habakuki UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002

UTANGULIZIInaonekana kwamba Habakuki alifanya kazi yake ya kinabii katika Yuda yapata mwaka wa 600 mbele ya Kristo. Huo ulikuwa wakati wa utawala wa mufalme Yehoyakini. Wakati huo Wababeli ndio taifa lililokuwa na nguvu kule Mashariki ya Kati na liliyagandamiza na kunyanganya mali za mataifa mengine, kati yao kulikiwa taifa la Yuda. Habakuki alipinga jambo hilo la kuonea wadogo na taifa baya lenye zambi. Kwa nini (Mungu) unanyamaza waovu wanapowamaliza wale watu wanaokuwa wenye haki kuliko wao? (1.13). Jibu la Mungu ni kwamba yeye atafanya kitu wakati wake na mpaka wakati huo: Uwaangalie wenye kiburi, hao wataangamia; lakini wenye haki wataishi kwa kumwamini Mungu (2.4).Sehemu ya mwisho ya kitabu hiki ni maombi, na katika maombi hayo nabii anaeleza ukubwa wa Mungu, kisha anakumbusha juu ya imani kwa Mungu.
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help