1Mufalme Yosia akafanyia Yawe sikukuu ya Pasaka katika Yerusalema, wakachinja wana-kondoo wa Pasaka siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza.
2Akawaweka makuhani kwa kazi zao ambazo walihitajika kufanya katika nyumba ya Yawe na kuwatia moyo wazifanye kwa ukamilifu.
3Pamoja na hayo, akawapa Walawi waliowafundisha watu wa Israeli na ambao walitakaswa kwa ajili ya Yawe, maagizo haya: “Muweke Sanduku takatifu ndani ya nyumba ambayo Solomono mwana wa Daudi, mufalme wa Israeli aliyojenga; hamuhitaji kulibebabeba tena juu ya mabega. Sasa mumutumikie Yawe, Mungu wenu, na watu wake Waisraeli.
4Mushike kazi yenu kulingana na ukoo zenu, kufuatana na maagizo ya Daudi mufalme wa Israeli na ya Solomono mwana wake. Ang. 2 Sik 8.14
5Musimame vilevile Pahali Patakatifu kama vile wasimamizi wa jamaa za ukoo zenu wasiofanya kazi za ukuhani, na kila mumoja asimamie jamaa moja ya Walawi.
6Muchinje mwana-kondoo wa Pasaka, mujitakase, halafu mutayarishe Pasaka kwa ajili ya wandugu zenu, kusudi waweze kutimiza neno la Yawe lililosemwa na Musa.”
7Kisha Yosia akawapa watu, wana-mbuzi yapata elfu makumi tatu, na ngombe dume elfu tatu, wote hawa toka katika makundi ya mufalme.
8Nao wakubwa wake, kwa mapenzi yao, waliwapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zakaria na Yehieli, wasimamizi wa nyumba ya Mungu, waliwapa makuhani wana-kondoo na wana-mbuzi elfu mbili mia sita na ngombe dume mia tatu kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
9Naye Konania na wandugu zake wawili, Semaya na Netaneli, pamoja na Hasabia, Yeieli na Yozabadi, waliokuwa viongozi wa Walawi, nao vilevile waliwapa wana-kondoo na wana-mbuzi elfu tano na ngombe dume mia tano, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
10Basi utaratibu wa kazi ukapangwa, makuhani wakasimama pahali pao, na Walawi katika makundi yao; sawasawa na amri ya mufalme.
11Wakachinja mwana-kondoo wa Pasaka, nao makuhani wakanyunyiza damu waliyopokea kwa mikono yao nao Walawi wakachuna nyama.
12Halafu wakatenga sadaka za kuteketeza kwa moto kusudi wapate kuzigawanya kwa watu kulingana na jamaa zao kusudi wamutolee Yawe kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa. Nao wakafanya vile vile na wale ngombe dume.
13Wakachoma mwana-kondoo wa Pasaka juu ya moto kufuatana na maagizo; vilevile wakatokotesha sadaka takatifu katika vyungu, masufuria na kwenye vikaango, na kuwagawanyia upesiupesi watu wasiofanya kazi ya ukuhani. Ang. Kut 12.8-9
14Kisha, Walawi wakafanya matayarisho kwa ajili yao wenyewe na kwa makuhani kwa maana makuhani wa uzao wa Haruni walikuwa wanashugulika na kutoa sadaka za kuteketeza kwa moto, na vipande vya mafuta, mpaka usiku; kwa hiyo Walawi walitayarisha kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Haruni.
15Nao waimbaji wa uzao wa Asafu wakashika nafasi zao, kufuatana na maagizo ya mufalme Daudi, Asafu, Hemani na Yedutuni, nabii wa mufalme. Nao walinzi wa mulango walikuwa kwenye milango; hawakuhitajika kuacha nafasi zao za kazi kwa sababu wandugu zao Walawi waliwatayarishia Pasaka. Ang. 1 Sik 25.1
16Hivyo basi, kazi yote ya Yawe ikatayarishwa siku hiyo, kwa kufanya Pasaka na kutoa sadaka za kuteketeza kwenye mazabahu ya Yawe; kama vile mufalme Yosia alivyoamuru.
17Wakati ule watu wote wa Israeli waliokuwa pale walifanya sikukuu hiyo ya Pasaka na sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa muda wa siku saba. Ang. Kut 12.1-20
18Pasaka kama hiyo ilikuwa haikufanyika katika Israeli yote tangu siku za nabii Samweli. Hakujatokea mufalme hata mumoja wa Israeli aliyefanya Pasaka kama hii iliyofanyika na mufalme Yosia, makuhani, Walawi na watu wote wa inchi ya Yuda, wa Israeli vilevile na wakaaji wa Yerusalema.
19Pasaka hiyo ilifanyika katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa mufalme Yosia.
Mwisho wa utawala wa Yosia(2 Fal 23.28-30)20Nyuma ya haya yote mufalme Yosia aliyofanya kwa ajili ya hekalu, Neko, mufalme wa Misri akapanda kwenda kushambulia Karkemisi kwenye muto Furati. Naye mufalme Yosia akatoka kwa kumushambulia,
21lakini mufalme Neko akamutumia ujumbe akisema: “Vita hivi havikuelekei wewe hata kidogo, ewe mufalme wa Yuda. Sikukuja kupigana nawe lakini na waadui zangu, na Mungu ameniamuru niharakishe. Acha basi kumupinga Mungu, ambaye yuko upande wangu, kama sivyo atakuangamiza.”
22Lakini Yosia hakukubali kumwachilia. Akakataa kusikiliza maneno Mungu aliyosema kwa njia ya Neko, kwa hiyo akajibadilisha kusudi asitambulikane, kisha akaingia katika vita katika bonde la Megido.
23Nao wapiga upinde wakamuchoma mufalme Yosia mishale; basi mufalme akawaambia watumishi wake: “Muniondoshe! Nimeumia vibaya sana.”
24Basi watumishi wake walipomutoa katika gari lake la vita, wakamubeba na gari lake la pili mpaka Yerusalema. Naye akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme. Watu wote wa inchi ya Yuda na Yerusalema wakaomboleza kifo cha Yosia.
25Nabii Yeremia vilevile akatunga shairi la maombolezo kwa ajili ya kifo chake; nao waimbaji wote, wanaume na wanawake, wanamutaja Yosia katika maombolezo yao, mpaka leo. Wakakusudia kuwa wanafanya maombolezo haya katika Israeli; angalia nayo yameandikwa katika Maombolezo.
26Matendo mengine ya Yosia na matendo yake mema kama vile yalivyoandikwa katika Sheria ya Yawe,
27na matendo yake tangu mwanzo mpaka mwisho, angalia yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na Yuda.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.