Zaburi 46 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu yuko upande wetu

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa.

2Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu;

yeye ni musaada wetu wakati wa taabu.

3Kwa hiyo hatutaogopa kitu chochote,

hata dunia ikiyeyuka

na milima kutikisika kutoka bahari,

4hata kama bahari ikichafuka na kutisha,

na milima ikitetemeka kwa machafuko yake.

5Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu,

makao matakatifu ya Mungu Mukubwa.

6Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa;

Mungu ataupatia musaada kila asubui.

7Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika;

Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.

8Yawe wa majeshi yuko pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.

9Mukuje muone matendo ya Yawe.

Muone maajabu aliyofanya katika dunia.

10Anakomesha vita popote katika dunia.

Anavunjavunja pinde na mikuki,

nayo magari ya vita anayateketeza.

11Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu!

Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote;

mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”

12Yawe wa majeshi yuko pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help