1Musikilize maombolezo yangu juu yenu,
enyi Waisraeli:
2Umeanguka na hautainuka tena
ewe binti Israeli!
Umeachwa ukiwa katika inchi yako,
hakuna hata mutu wa kukuinua.
3Maana Bwana wetu Yawe anasema:
Itakuwa hivi: juu yenu ninyi Waisraeli:
Watu elfu moja wanatoka katika muji kwenda kupigana
lakini watarudia watu mia moja tu;
wataondoka watu mia moja wa kijiji kimoja
lakini watu kumi tu wataponyoka.
4Yawe anawaambia Waisraeli hivi:
Munitafute mimi nanyi mutaishi!
5Lakini musinitafutie kule Beteli
wala musiende Gilgali
wala musivuke kwenda Beri-Seba.
Maana wakaaji wa Gilgali,
hakika watapelekwa katika uhamisho,
na Beteli utaangamizwa!
6Mutafute Yawe, nanyi mutaishi!
Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto;
moto utawateketeza wakaaji wa Beteli
na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha.
7Angalisho, enyi munaogeuza sheria kuwa uchungu,
na kuona haki kuwa kama takataka!
8Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni,
ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana,
na muchana kuwa usiku;
yeye anayekusanya maji ya bahari
na kuyamwanga juu ya inchi kavu,
Yawe ndilo jina lake.
9Yeye ndiye anayewaangamiza wenye nguvu,
na kuziharibu kuta zao zenye nguvu.
10Ninyi munawachukia wanaotetea haki
na wenye kusema ukweli katika tribinali.
11Ninyi munawagandamiza wazaifu
na kuwalipisha kodi ya ngano.
Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa,
lakini ninyi hamutaishi humo;
munalima bustani nzuri za mizabibu,
lakini hamutakunywa divai yake.
12Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu
na ukubwa wa zambi zenu;
ninyi munawatesa watu wema,
munapokea kituliro
na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.
13Basi, kutakuwa wakati mubaya
ambao hata mwenye hekima atanyamaza.
14Mutafute kutenda mazuri wala si mabaya,
kusudi ninyi mupate kuishi
naye Yawe wa majeshi
atakuwa pamoja nanyi kama vile munavyosema.
15Muchukie mabaya, mupende mazuri,
na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali.
Labda Yawe wa majeshi
atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.
16Basi, Yawe, Mungu wa majeshi,
Bwana wetu anasema hivi:
Kutakuwa kilio kila nafasi katika barabara za muji;
watu wataomboleza: Ole! Ole!
Walimaji wataitwa kuja kuomboleza,
na wafundi wa kuomboleza kuja kufanya kilio.
17Kutakuwa kilio katika mashamba yote ya mizabibu;
maana nitapita kati yenu kwa kuwaazibu.
Ni Yawe anayesema hivyo.
Siku ya Yawe18Ole kwenu ninyi munaoingojea kwa hamu
siku ya Yawe!
Kwa nini munaitaka sana siku hiyo?
Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na si ya mwangaza!
19Mambo yatakuwa kama mutu aliyekimbia simba,
halafu anakutana na dubu!
Au kama mutu anayerudi kwa nyumba yake,
na kutia mukono wake kwenye ukuta, na kuumwa na nyoka.
20Siku ya Yawe itakuwa giza, na si mwangaza;
itakuwa giza kubwa bila mwangaza wowote.
21Yawe anasema hivi:
Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu;
siifurahii mikutano yenu ya kidini.
22Hata mukinitolea sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na za vyakula,
mimi sitakubali kuzipokea;
na sadaka zenu za amani za nyama wanono
mimi sitaziangalia kabisa.
23Muondoe mbele yangu kelele za nyimbo zenu!
Sitaki kusikiliza muziki wa vinubi vyenu!
24Lakini muache haki itiririke kama maji,
usawa ukuwe kama muto usiokauka.
25Enyi Waisraeli, wakati ule mulipokuwa kule katika jangwa kwa miaka makumi ine, muliniletea matoleo na sadaka hata mara moja?
26Mulibeba kama vile sasa sanamu za mungu wenu Sakuti mufalme wenu na sanamu za Kiuni mungu wenu wa nyota, vitu ambavyo mulijitengenezea wenyewe?
27Kwa hiyo nitawapeleka katika uhamisho, mbali kuliko Damasiki!
–Ni Yawe anayesema, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.