1Kutatokea chipukizi katika shina la Yese,
tawi litachipuka toka mizizi yake.
2Roho wa Yawe atakaa kwake,
Roho wa hekima na maarifa,
Roho wa shauri jema na nguvu,
Roho wa akili na utii wa Mungu.
3Furaha yake itakuwa kumutii Yawe.
Hatatoa hukumu kulingana na yale anayoona,
wala kuamua kufuatana na yale anayosikia.
4Atawaamulia wamasikini kwa haki
na kutetea haki za wakosefu katika inchi.
Kwa neno lake dunia itaazibiwa,
kwa pumzi yake waovu watauawa.
5Haki itakuwa kama mukaba wa kujifunga,
uaminifu utakuwa kama mukaba kwenye kiuno chake.
6Imbwa wa pori ataishi pamoja na mwana-kondoo,
chui atapumzika pamoja na mwana-mbuzi.
Wana-ngombe na wana-simba watakula pamoja,
na mutoto mudogo atawaongoza.
7Ngombe na dubu watakula pamoja,
watoto wao watapumzika pamoja;
na simba atakula majani kama ngombe.
8Mutoto muchanga atacheza kwenye shimo la nyoka,
mutoto ataweza kutia mukono kwenye shimo la nyoka wa sumu.
9Katika mulima mutakatifu wa Mungu
hakutakuwa ubaya wala uharibifu.
Maana kumujua Yawe kutaenea pote katika inchi,
kama vile maji yanavyojaa katika bahari. Wanaokuwa katika uhamisho watarudia
10Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka. Ang. Rom 15.12
11Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.
12Naye atasimika bendera kuwaita mataifa,
kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa,
kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa,
na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.
13Wivu wa Efuraimu juu ya Yuda utakoma,
hakutakuwa tena uadui kati ya Yuda na Efuraimu.
14Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi,
pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki.
Watawashinda Waedomu na Wamoabu,
nao Waamoni watawatii.
15Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri,
kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati,
nao utagawanyika katika vijito saba,
watu wavuke humo miguu mikavu.
16Tena, kutakuwa barabara kubwa toka Asuria
kwa ajili ya watu wake waliobaki humo
kama ilivyokuwa kwa Waisraeli
wakati walipotoka katika inchi ya Misri.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.