1Basi Yawe akamutuma nabii Natani kwa Daudi. Natani alimwendea Daudi, akamwambia: “Kulikuwa wanaume wawili katika muji mumoja. Mumoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa masikini.
2Yule tajiri alikuwa na kondoo wengi na ngombe wengi.
3Lakini yule masikini alikuwa na mwana-kondoo mudogo mumoja dike, ambaye alikuwa amemununua. Alimutunza, naye akakomaa katika nyumba yake pamoja na watoto wake. Alimukulisha mwana-kondoo yule chakula kilekile kama chake na kunywea kwenye kikombe chake naye vilevile alikuwa akimukumbatia kwenye kifua. Mwana-kondoo yule alikuwa kama binti kwa yule mutu masikini.
4Siku moja, yule tajiri alifikiwa na mugeni. Basi, tajiri yule hakutaka kukamata kondoo mumoja kati ya kondoo wake mwenyewe au ngombe wake, amuchinjie mugeni wake, lakini alikwenda na kumunyanganya yule masikini mwana-kondoo wake, akamuchinjia mugeni wake.”
5Daudi aliposikia hayo, akawaka hasira juu ya yule tajiri. Akamwambia nabii Natani: “Kama vile Yawe anavyoishi, mutu aliyefanya jambo hilo anastahili kufa!
6Naye anapaswa kumurudishia yule masikini mwana-kondoo yule, tena mara ine, maana ametenda jambo baya na hakukuwa na huruma!”
7Natani akamwambia Daudi: “Wewe ndiwe mutu yule! Sasa, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mimi nilikupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya Israeli. Nilikuokoa toka katika mikono ya Saulo.
8Nilikupa nyumba ya bwana wako na wake zake wakuwe wako, tena nikakupa watu wa Israeli na wa Yuda uwatawale. Na kama haya yangekuwa kidogo sana kwako ningekuongezea mara mbili zaidi ya hayo.
9Kwa nini basi, umezarau neno langu mimi Yawe na kufanya uovu huu mbele yangu? Umemwua Uria wa Hiti kwa upanga, ukamukamata muke wake kuwa muke wako. Umewatumia Waamoni kwa kumwua Uria katika vita!
10Kwa hiyo basi, kwa sababu umenizarau na umemutwaa muke wa Uria wa Hiti kuwa muke wako, mauaji hayataondoka katika jamaa yako.’
11Sikiliza, Yawe anasema: ‘Nitaleta hasara katika jamaa yako mwenyewe. Nitawatwaa wake zako ukiona kwa macho yako mwenyewe na kumupa jirani yako, naye atalala nao waziwazi.
12Wewe ulifanya jambo hilo kwa siri, lakini mimi nitayafanya hayo mbele ya Waisraeli wote waziwazi.’ ”
13Basi, Daudi akamwambia Natani: “Nimetenda zambi mbele ya Yawe.”
Natani akamwambia: “Yawe amekusamehe zambi yako, nawe hautakufa.
14Hata hivyo, kwa sababu kwa tendo lako umemuzarau kabisa Yawe, mutoto wako atakufa.”
15Kisha Natani akarudi kwake.
Mutoto wa Daudi anakufaYawe alimupiga mutoto ambaye Batiseba muke wa Uria alimuzalia Daudi, naye akakuwa mugonjwa.
16Daudi alimwomba Mungu kwa ajili ya mutoto yule. Akafunga kula chakula, akaingia ndani ya chumba chake, na usiku kucha akalala chini.
17Wazee wa nyumba yake walimufuata na kumusihi aamuke, lakini yeye alikataa, na hakukula chakula chochote pamoja nao.
18Nyuma ya juma moja, mutoto yule akakufa. Watumishi wa Daudi waliogopa kumwambia kwamba mutoto amekufa, maana walifikiri: “Mutoto yule alipokuwa angali muzima, tulizungumuza naye, lakini hakutusikiliza. Sasa, tutamwambia namna gani kama mutoto wake amekufa? Labda atajizuru.”
19Daudi alipowaona watumishi wake wananongonezana, akatambua kwamba mutoto wake amekufa. Kwa hiyo, akawauliza: “Mutoto amekufa?”
Nao wakamujibu: “Ndiyo! Amekufa.”
20Kisha, Daudi akasimama, akaoga, akajipakaa mafuta na kubadilisha nguo zake. Halafu akaenda katika nyumba ya Yawe na kuabudu. Kisha akarudi kwake, akaamuru wamuletee chakula, naye akakula.
21Halafu watumishi wake wakamwuliza: “Ni jambo gani hili ulilofanya? Mutoto alipokuwa muzima, wewe ulifunga na kumulilia. Lakini alipokufa, ukasimama, ukakula chakula.”
22Daudi akawajibu: “Ni kweli mutoto alipokuwa muzima, nilifunga na kulia. Nilifanya hivyo maana nilifikiri: ‘Nani anajua? Labda Yawe atanihurumia kusudi mutoto aishi’.
23Lakini sasa amekufa, kwa nini nifunge? Mimi ninaweza kumurudisha katika dunia? Siku moja, nitakwenda kule alikokwenda, lakini yeye hawezi kurudi kwangu.”
Kuzaliwa kwa Solomono24Halafu Daudi akamufariji Batiseba muke wake. Akalala naye, naye akapata mimba na kuzaa mutoto mwanaume, naye Daudi alimwita Solomono. Yawe alimupenda mutoto yule,
25naye akamutuma nabii Natani kwa Daudi kwamba amwite mutoto yule Yedidia, ni kusema “Anayependwa na Yawe”, kwa ajili ya Yawe.
Daudi anauteka muji wa Raba(1 Sik 20.1-3)26Wakati ule, Yoabu aliushambulia Raba muji wa Waamoni, naye akauteka muji ule wa kifalme.
27Yoabu akatuma ujumbe kwa Daudi: “Nimeushambulia muji wa Raba, nami nimekikamata kisima chao cha maji.
28Sasa uwakusanye watu wote waliobaki, upige kambi kwa kuuzunguka na kuuteka. Kama sivyo, nikiuteka, utaitwa kwa jina langu.”
29Kwa hiyo, Daudi akakusanya watu wote, akaenda Raba, akaushambulia na kuuteka muji ule.
30Kisha akatwaa taji ya mufalme wao kutoka kwenye kichwa chake. Uzito wa taji hiyo ya zahabu ulikuwa kilo makumi tatu na tano; na ndani yake mulikuwa jiwe la bei kali. Naye Daudi akavalishwa taji hiyo kwenye kichwa chake. Vilevile aliteka vitu vingi sana katika muji ule.
31Halafu aliwakamata watu wa muji ule, akawaweka kwa kazi ya kutumikisha misumeno, sururu za chuma, mashoka ya chuma na kuwatumia kufanya kazi katika furu ya matofali. Hivi ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote walirudi Yerusalema.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.