1Si lazima niwaandikie juu ya musaada unaotumwa kwa watu wa Mungu wanaokuwa katika Yudea.
2Kwa maana ninajua nia yenu nzuri ya kusaidia, nami ninajivuna kwa ajili yenu mbele ya watu wa Makedonia, nikisema: “Kanisa la jimbo la Akaya liko tayari kusaidia tangia mwaka jana.” Hivi kwa njia ya bidii yenu mumewavuta wengi kati yao kwa kutoa vilevile.
3Lakini sasa ninawatumia wandugu hawa kusudi kujisifu kwetu kwa ajili yenu kusionekane kuwa bure. Kwa hiyo ninataka mukuwe tayari kama vile nilivyosema.
4Kwa maana kama watu wa Makedonia wanakuja pamoja nami na tusipowakuta tayari, sisi tutapata haya sana kwa kuona jinsi nilivyowaaminia, nami sisemi kitu juu ya haya ambayo ninyi mutaweza kupata.
5Ni hivi niliona kuwa ni vizuri kuwashauri wandugu hawa watangulie kufika kwenu mbele yangu kusudi watayarishe vile vitu mulivyoahidi kutoa kwa mapenzi yenu. Hivi vitakuwa tayari na itaonyesha kwamba mumevitoa kwa moyo mwema, wala si kwa uchoyo.
6Mukumbuke maneno haya: yule anayepanda kidogo atavuna kidogo, na yule anayepanda kwa uwingi atavuna kwa uwingi.
7Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.
8Na Mungu anaweza kuwajalia mema ya kila namna, kusudi siku zote mupate vyote munavyohitaji, na hivi mupate kuzidi kutoshelewa katika kutenda kazi njema.
9Kama vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu:
“Ametoa kwa uwingi,
amewapa wamasikini.
Haki yake inadumu milele.”
10Mungu ndiye anayemupatia mupandaji mbegu na mukate wa kukula. Kwa hiyo atawapatia ninyi mbegu yoyote munayohitaji na kuiotesha, kusudi moyo wenu wa kutoa upate kuzaa matunda mengi.
11Hivi mutakuwa watajiri katika vitu vyote, kusudi siku zote muweze kuonyesha moyo wa kutoa, hata watu wengi watamushukuru Mungu kwa ajili ya musaada tunaowafikishia kutoka kwenu.
12Kwa maana kazi hii ya kutoa munayofanya haifai tu kwa kusaidia watu wa Mungu kusudi wapate vitu wanavyokosa, lakini vilevile kwa njia ile watu wengi wanamutolea Mungu shukrani.
13Kufuatana na ushuhuda wa kazi hii, watu watamutukuza Mungu kwa kuona jinsi munavyoonyesha utii wenu katika kushika Habari Njema ya Kristo. Vilevile wanamutukuza kwa kuona moyo wa kutoa munaokuwa nao katika kushirikiana mali yenu pamoja nao na sisi.
14Kwa hiyo watawaombea kwa upendo mwingi, kwa ajili ya neema kubwa sana Mungu aliyowajalia.
15Shukrani kwa Mungu kwa ajili ya zawadi yake inayopita kipimo!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.