Zaburi 121 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu ni mulinzi wetu

1Wimbo wa safari za kidini.

Ninainua macho kwenye milima.

Musaada wangu unatoka wapi?

2Musaada wangu unatoka kwa Yawe,

aliyeumba mbingu na dunia.

3Hatakuacha uanguke;

mulinzi wako hasinzii.

4Kweli mulinzi wa Israeli

hasinzii wala halali.

5Yawe ni mulinzi wako;

yuko upande wako wa kuume kwa kukukinga.

6Muchana jua halitakuchoma,

wala mwezi hautakuzuru usiku.

7Yawe atakukinga na uovu wote;

atayalinda salama maisha yako.

8Yawe atakulinda katika shuguli zako zote

tangu sasa na hata milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help