1Zaburi ya Daudi.
Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe;
ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake.
2Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari;
aliisimika imara juu ya maji mengi.
3Nani atakayepanda kwa mulima wa Yawe?
Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?
4Ni mutu wa matendo mema na moyo safi,
asiyefuata mambo ya ovyo,
wala kuapa kwa uongo.
5Mutu huyo atapokea baraka kwa Yawe,
na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.
6Ndiyo hali ya kizazi cha watu wanaomutafuta yeye,
watu wanaomutafuta Mungu wa Yakobo.
7Mufunguke, enyi milango;
mufunguke, enyi milango ya tangia zamani,
kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.
8Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu?
Ni Yawe, mwenye nguvu na uwezo;
Yawe, mwenye uwezo katika vita.
9Mufunguke, enyi milango,
mufunguke, enyi milango ya tangia zamani,
kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.
10Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu?
Ni Yawe, wa majeshi,
yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.