1Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!
2Na kama wakikuuliza: Tutaenda wapi? Wewe utawajibu kwamba:
Yawe anasema hivi:
Walioandikiwa kufa kwa ugonjwa mukali, watakufa kwa ugonjwa mukali,
walioandikiwa kufa kwa vita, watakufa kwa vita,
walioandikwa kufa kwa njaa, watakufa kwa njaa;
nao walioandikiwa kupelekwa katika utumwa, watapelekwa katika utumwa.
3Nimeamua kuleta aina ine za maangamizi juu yao: upanga kwa kuwaua, imbwa kwa kuwararua, ndege na nyama wa pori kwa kuwakula na kuwamaliza.
4Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha kwa falme zote za dunia, kwa sababu ya mambo ambayo Manase mwana wa Hezekia, aliyofanya kule Yerusalema, alipokuwa mufalme wa Yuda.
–Ni ujumbe wa Yawe.
5Ni nani atakayewahurumia, enyi watu wa Yerusalema?
Ni nani atakayeomboleza juu yenu?
Nani atasimama kuuliza habari zenu?
6Ninyi mumenikataa mimi.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Ninyi mumeniacha na kurudi nyuma.
Kwa hiyo nimenyoosha mukono kwa kuwaangamiza.
Nimechoka na kuwahurumia.
7Nimepepeta watu wangu
kwa kuwasambaza sawa maganda,
toka katika kila muji wa inchi yao.
Nimewaangamiza kwa kuwaua watoto wao,
lakini hawakuacha mwenendo wao.
8Wajane wao wamekuwa wengi
kuliko muchanga wa bahari.
Nao wamama wenye watoto vijana
nimewaletea mwangamizaji muchana kati.
Nimesababisha uchungu na vitisho
viwapate kwa rafla.
9Mama aliyeheshimiwa kwa kuwa na watoto saba,
sasa kwa rafla hana kitu.
Amezimia na kukata roho,
amekufa angali kijana,
amefezeheka na kuzarauliwa.
Na wale watakaobaki wazima
nitawatoa kwa upanga mbele ya waadui zao.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Yeremia anamulalamikia Mungu10Ole wangu, mama yangu, kwa sababu ulinizaa! Mimi nimekuwa mutu wa ubishi na ugomvi katika inchi yote! Sijapata kukopesha mutu wala kukopeshwa na mutu, lakini kila mutu ananilaani.
11Basi, ee Yawe, acha laana hizo zinipate kama sikukutumikia vizuri na kama sikukusihi kwa ajili ya waadui zangu wakati walipokuwa katika taabu na shida!
12Mutu anaweza kuvunja chuma, kile chuma au shaba inayotoka kaskazini?
13Yawe anasema: Nitazifanya mali zenu na akiba zenu zitekwe tena, wala hamutapewa malipo yoyote ya vitu hivyo kwa sababu ya zambi zenu zote mulizozitenda kila pahali katika inchi.
14Nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.
15Nami nikasema:
Lakini wewe Yawe unanielewa vizuri;
unikumbuke na kuja kunisaidia.
Unilipizie watesaji wangu kisasi.
Wewe ni muvumilivu, usiniache niangamie;
kumbuka kwamba ninatukaniwa kwa ajili yako.
16Palepale maneno yako yaliponifikia, niliyameza;
nayo yakanifurahisha,
yakakuwa matamu katika moyo wangu,
maana mimi ninajulikana kwa jina lako,
ee Yawe wa majeshi.
17Mimi sikuikaa pamoja na wanaojifurahisha,
wala sikufurahi pamoja nao.
Niliikaa peke yangu nikilemewa na nguvu yako;
kwa maana ulinijaza hasira yako.
18Kwa nini mateso yangu hayaishi?
Mbona kidonda changu hakiponi
nacho hakitaki kutunzwa?
Kama vile kijito chenye kukaukakauka,
kisivyoweza kutumainiwa,
ndivyo wewe umekuwa kwangu!
19Basi, Yawe akasema hivi:
Kama ukinirudilia, nitakurudisha katika hali yako ya mbele,
nawe utanitumikia tena.
Kama ukisema maneno ya maana, yasiyokuwa ya upuuzi,
basi utakuwa musemaji wangu.
Watu watakufikia wewe,
wala si wewe utakayehitaji kuwaendea.
20Mbele ya watu hawa,
nitakufanya sawa ukuta mugumu wa shaba.
Watapigana nawe,
lakini hawataweza kukushinda,
maana, mimi niko pamoja nawe,
nipate kukuokoa na kukukomboa.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
21Nitakuokoa toka katika mikono ya watu waovu,
na kukuopoa toka katika makucha ya watesaji.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.